Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 6:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Hamani alipoingia ndani, mufalme akamwuliza: “Nimufanyie nini mutu ambaye ningependa sana kumupatia heshima?” Hamani akafikiri ndani ya moyo wake: “Ni nani huyo ambaye mufalme angependa kumupatia sana heshima? Bila shaka ni mimi.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 6:6
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akawauliza hivi: “Kulingana na sheria, malkia Vashiti afanyiwe nini? Maana, nimewatuma matowashi wangu kwake, lakini yeye amekataa kuitii amri yangu, mimi mufalme Ahasuero!”


Halafu akaanza kueleza juu ya utajiri anaokuwa nao, wana anaokuwa nao, jinsi mufalme alivyomupandisha cheo, na jinsi alivyopewa madaraka zaidi kuliko wakubwa wengine wote wa mufalme.


Basi, Hamani akatwaa nguo zile na kumuvalisha Mordekayi, akamutembeza kwenye kiwanja cha muji akiwa juu ya farasi wa mufalme, naye akitangaza: “Hivi ndivyo anavyotendewa mutu ambaye mufalme amependa kumupa heshima.”


Basi, watumishi wakamujibu mufalme: “Hamani yuko katika kiwanja.” Mufalme akasema: “Mumukaribishe ndani.”


Basi, Hamani akamujibu mufalme: “Mutu huyo ambaye mufalme angependa kumupatia heshima,


na mumoja wa washauri wako wa kuheshimika ee mufalme amuvalishe mutu yule nguo hizo za kifalme, na kumwongoza mutu yule akiwa amepanda juu ya farasi wako mpaka kwenye kiwanja cha muji, naye akitangaza: ‘Hivi ndivyo anavyotendewa mutu ambaye mufalme amependa kumupa heshima.’ ”


Lakini wanaotaka kuona kwamba sina kosa, wakuwe na furaha tele, waseme siku zote: “Yawe ni mukubwa! Anapendezwa na kumupatia mutumishi wake uheri.”


Maana wajinga wanajiua kwa kiburi chao, wapumbafu wanajiangamiza kwa kufanikiwa kwao.


Kiburi kinatangulia maangamizi; majivuno yanatangulia maanguko.


Majivuno ya ndani ya moyo yanaleta maangamizi, lakini unyenyekevu unaleta heshima.


Kuna watu ambao macho yao yanajaa kiburi. Wanazarau kila kitu wanachoona.


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Nitafurahi kuwatendea mema; nitawasimika siku zote katika inchi hii na kuwatendea kwa uaminifu.


Kiburi chako kimekudanganya: wewe unayekaa ndani ya mashimo chini ya mawe makubwa na makao yako yapo juu kwenye milima, hivyo unajisemesha: Nani anayeweza kunishusha chini?


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Naye anapokuja, yule aliyewaalika ninyi wawili, ataweza kuja kukuambia: ‘Umwachie mutu huyu kiti.’ Halafu utapatwa na haya kwenda kuikaa kwenye viti vya nyuma.


kusudi watu wote wamuheshimu Mwana kama vile wanavyomuheshimu Baba. Asiyemuheshimu Mwana, hamuheshimu Baba aliyemutuma.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ