Mufalme akauliza: “Kuna mukubwa yeyote katika kiwanja?” Ikakuwa wakati ule Hamani alikuwa ameingia katika kiwanja cha inje cha nyumba ya kifalme; alikuwa amekuja kwa mufalme kuomba Mordekayi auawe kwenye muti ambao alikuwa amekwisha kumutayarishia.
Hamani alipoingia ndani, mufalme akamwuliza: “Nimufanyie nini mutu ambaye ningependa sana kumupatia heshima?” Hamani akafikiri ndani ya moyo wake: “Ni nani huyo ambaye mufalme angependa kumupatia sana heshima? Bila shaka ni mimi.”