Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 6:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mufalme akauliza: “Kuna mukubwa yeyote katika kiwanja?” Ikakuwa wakati ule Hamani alikuwa ameingia katika kiwanja cha inje cha nyumba ya kifalme; alikuwa amekuja kwa mufalme kuomba Mordekayi auawe kwenye muti ambao alikuwa amekwisha kumutayarishia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 6:4
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Watumishi wote wa mufalme na watu wote wa majimbo yote wanajua kwamba mutu yeyote yule akiingia katika kiwanja cha ndani na kumwona mufalme bila kuitwa, huyo anapaswa kuuawa. Anayeweza kuponyoka ni yule tu ambaye mufalme atamunyooshea fimbo yake ya zahabu kwa kumuponyesha. Na mimi sijaitwa na mufalme, yapata mwezi muzima sasa.”


Kisha siku tatu ya kufunga kwake, Esteri akavaa nguo zake za kimalkia, akaenda kusimama katika kiwanja cha ndani cha nyumba ya mufalme, kuelekea chumba cha mufalme. Mufalme alikuwa mule ndani akiikaa katika kiti chake cha kifalme, kuelekea mulango wa nyumba ya mufalme.


Basi, muke wake Zeresi na warafiki zake wakamushauria hivi: “Kwa nini asitengenezewe muti wa kutundikia, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili? Kesho asubui, unaweza kuzungumuza na mufalme kusudi Mordekayi auawe juu yake, kisha uende ukule karamu na mufalme kwa furaha.” Wazo hilo lilimufurahisha Hamani, naye akatengeneza muti ule.


Mufalme akauliza: “Tumemupa Mordekayi heshima au sifa gani kwa jambo hili?” Watumishi wake wakamujibu: “Hajafanyiwa jambo lolote.”


Basi, watumishi wakamujibu mufalme: “Hamani yuko katika kiwanja.” Mufalme akasema: “Mumukaribishe ndani.”


Harbona, mumoja wa wale matowashi waliomutumikia mufalme, akasema: “Hamani amesubutu hata kutengeneza muti wa kumutundikia Mordekayi ambaye aliyaokoa maisha yako, ewe mufalme. Muti huo, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili, bado uko kule katika nyumba yake.” Hapo mufalme akaamuru: “Mumutundike Hamani juu ya muti uleule.”


Anawanasa wenye hekima kwa werevu wao, anakomesha mara moja mipango ya waovu.


Yule anayetawala juu mbinguni anawachekelea na kuwazarau.


Yeye anawaokoa katika kifo, anawalinda wakati wa njaa.


Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ