Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 6:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mufalme akauliza: “Tumemupa Mordekayi heshima au sifa gani kwa jambo hili?” Watumishi wake wakamujibu: “Hajafanyiwa jambo lolote.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 6:3
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, yule mutunza vinywaji mukubwa akamusahau Yosefu, pahali pa kumukumbuka.


Halafu Daudi akasema: “Mutu atakayetangulia kuwapiga Wayebusi, atakuwa mukubwa na jemadari katika jeshi.” Basi Yoabu mwana wa Zeruya, akakuwa wa kwanza kuwashambulia, hivyo akakuwa mukubwa.


Ikaonekana jinsi ilivyoandikwa ikielezwa jinsi Mordekayi alivyopasha habari ya shauri la kumwua mufalme iliyokuwa imefanywa na Bigitani na Teresi, hao wawili kati ya matowashi wa mufalme waliokuwa walinzi wa vyumba vya mufalme.


Mufalme akauliza: “Kuna mukubwa yeyote katika kiwanja?” Ikakuwa wakati ule Hamani alikuwa ameingia katika kiwanja cha inje cha nyumba ya kifalme; alikuwa amekuja kwa mufalme kuomba Mordekayi auawe kwenye muti ambao alikuwa amekwisha kumutayarishia.


Katika muji ule, kulikuwa masikini mumoja mwenye hekima ambaye, kwa hekima yake, aliokoa muji ule. Lakini hakuna mutu aliyemukumbuka yule masikini kisha.


Lakini, nimesikia kwamba wewe unaweza kueleza vitendawili na kutambua mafumbo. Basi, kama ukiweza kusoma maandiko haya na kunielezea maana yake, utavalishwa nguo nzuri ya rangi nyekundu na kuvalishwa mukufu wa zahabu katika shingo lako. Utapewa nafasi ya tatu katika ufalme huu.


Pale pale, mufalme Belsasari akaamuru kwamba Danieli avalishwe nguo nzuri nyekundu na mukufu wa zahabu katika shingo. Ikatangazwa kwamba Danieli atakamata sasa nafasi ya tatu katika ufalme.


Mufalme Belsasari akaamuru kwa sauti kwamba wachawi, Wakaldea wenye hekima na waaguzi waletwe. Walipoletwa, mufalme akawaambia wenye hekima hao wa Babeli: Yeyote atakayesoma maandiko haya na kunijulisha maana yake, atavalishwa nguo nzuri nyekundu za kifalme na mukufu wa zahabu katika shingo lake, na kupewa nafasi ya tatu katika ufalme.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ