Basi, akamwita Hataki, mumoja wa matowashi wa mufalme aliyechaguliwa na mufalme amutumikie Esteri, akamutuma kwa Mordekayi kuuliza maneno na maana ya tukio hilo.
Akamupa na barua moja ya tangazo lililokuwa limetolewa katika muji wa Susani juu ya kuangamizwa kwa Wayuda, akamwomba amupelekee Esteri na kumwelezea jinsi hali inavyokuwa, na kumwambia aende kumusihi mufalme na kumwomba awahurumie Wayuda, watu wa Esteri.