Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 4:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Basi, akamwita Hataki, mumoja wa matowashi wa mufalme aliyechaguliwa na mufalme amutumikie Esteri, akamutuma kwa Mordekayi kuuliza maneno na maana ya tukio hilo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 4:5
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku ya saba ya karamu hiyo, mufalme Ahasuero akiwa amejaa furaha kutokana na divai aliyokuwa amekunywa, akawaita matowashi saba waliomutumikia yeye mwenyewe: Mehumani, Bizita, Harbona, Bigita, Abagita, Zetari na Karkasi.


Lakini Vashiti akakataa kufika kwa amri mufalme aliyotoa kwa njia ya matowashi. Kwa hiyo, mufalme akakasirika sana na hasira yake ikawaka.


Naye Esteri akamwambia Hataki arudie amwambie Mordekayi:


Malkia Esteri alipoarifiwa na matowashi na wajakazi wake habari za Mordekayi akahuzunika sana. Akamupelekea Mordekayi nguo za kuvaa kwa pahali pa nguo ya gunia, lakini Mordekayi akazikataa.


Hataki akamwendea Mordekayi katika uwanja, mbele ya mulango wa nyumba ya kifalme.


Hataki akaenda akamwelezea Esteri maneno yote Mordekayi aliyosema.


Mufurahi pamoja na wenye kufurahi. Mulie pamoja na wenye kulia.


Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote vinaugua pamoja nacho. Kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vingine vyote vinafurahi pamoja nacho.


Kila mutu asitafute faida yake mwenyewe, lakini atafute faida ya watu wengine.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ