Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 4:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 “Kwenda uwakusanye pamoja Wayuda wote wanaokuwa katika muji wa Susani. Mufunge, musikule wala musikunywe kwa siku tatu, usiku na muchana, kwa ajili yangu. Na mimi na wajakazi wangu tutafanya vile vile. Kisha, nitamwendea mufalme, ingawa ni kinyume cha sheria. Kama ni kuuawa, niuawe.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 4:16
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nimemuchagua yeye na wazao wake. Yeye atawafundisha wazao wake kushika njia yangu kwa kutenda kwa haki na kwa kufuata sheria yangu, nami nitawatimizia ahadi zangu.”


Mungu Mwenye Nguvu awajalie kupata huruma mbele ya mutu yule, awaachie yule ndugu yenu mwingine na Benjamina warudi pamoja nanyi. Kwa upande wangu, ikinipasa kupotelewa na wana wangu, basi!”


Lakini ujipe moyo! Tupigane kama wanaume kwa ajili ya watu wetu na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu. Naye Yawe atutendee lile analoona ni jema kwake.”


Hakuna maana ya kuingia katika muji kwa sababu kule tutakufa. Kwa hiyo kumbe tuende kwenye kambi ya Waaramu. Kama wakituacha kuishi, tutaishi; kama wakituua, tutakufa tu.”


Yosafati akashikwa na woga, akamwomba Yawe amwongoze. Akatangaza kwamba watu wote katika inchi ya Yuda wafunge kula.


Kisha, nikatoa maagizo kuwa sisi wote tufike karibu na muto Ahara kusudi tufunge kula chakula na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wetu na kumwomba atulinde na kutuongoza katika safari yetu pamoja na watoto wetu.


Basi, Mordekayi akaenda zake na kufanya kama vile Esteri alivyomwambia.


Katika kila jimbo, mara tu amri ya mufalme ilipotangazwa, kilio kikubwa kiliwapata Wayuda. Wakafunga, wakalia na kuomboleza; na wengi wao wakalala katika majivu wakiwa wamevaa magunia.


Kisha siku tatu ya kufunga kwake, Esteri akavaa nguo zake za kimalkia, akaenda kusimama katika kiwanja cha ndani cha nyumba ya mufalme, kuelekea chumba cha mufalme. Mufalme alikuwa mule ndani akiikaa katika kiti chake cha kifalme, kuelekea mulango wa nyumba ya mufalme.


na kuwaamuru wao na wazao wao washike sikukuu za Purimu kwa wakati wake uliopangwa, kama vile walivyokuwa wanazikumbuka sheria za kufunga wakati wa kuomboleza. Maagizo haya yalitolewa na Mordekayi, Muyuda, pamoja na malkia Esteri.


Siku hiyo, Yawe wa majeshi alitaka mulie na kuomboleza, munyoe nywele na kuvaa nguo za gunia.


Katika mwaka wa tano wa utawala wa mufalme Yoyakimu wa Yuda mwana wa Yosia, katika mwezi wa kenda, wakaaji wote wa Yerusalema na watu wote waliofika Yerusalema kutoka miji ya Yuda, walitangaza siku ya kufunga kula chakula mbele ya Yawe.


Aliwaambia wamwombe Mungu wa mbinguni awaonee huruma juu ya fumbo hilo, kusudi wao wasiangamie pamoja na wenye hekima wengine wa Babeli.


Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.


Kwa maana mutu anayetaka kulinda uzima wake ataupoteza; lakini yule atakayetoa uzima wake kwa ajili yangu ataulinda.


Pilato akajibu: “Yale niliyoandika, yameandikwa!”


Yule malaika aliyesema na Kornelio alipoondoka, akawaita watu wawili kati ya watumishi wake na askari mumoja mwenye kuogopa Mungu, aliyekuwa mumoja wa wasimamizi wake wa kipekee.


Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.


Lakini Paulo akajibu: “Kwa sababu gani munalia na kunivunja moyo? Mimi niko tayari, si kwa kufungwa tu kule Yerusalema, lakini hata kufa vilevile kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”


Usiku ulipokaribia kucha, Paulo akawasihi watu wote kula chakula, akisema: “Sasa leo ni siku ya kumi na ine tangu mulipobaki bila kula kitu chochote.


Akabaki muda wa siku tatu pasipo kuona, naye hakukula wala kunywa kitu.


Wao walijitolea kufa kwa kuokoa maisha yangu. Ninawashukuru, wala si mimi peke yangu tu, nayo makanisa yote ya inchi za watu wa mataifa wanawashukuru vilevile.


kwa sababu yeye alikuwa karibu kufa kwa ajili ya kazi ya Kristo. Alihatarisha maisha yake kwa kuja kuniletea musaada ule ambao ninyi wenyewe musingeweza kunipatia.


Kama hamutaki kumutumikia Yawe, basi muchague leo hii ni nani mutakayemutumikia: kama ni miungu ile ambayo wazee wenu waliitumikia ngambo ya muto Furati, au miungu ya Waamori ambao sasa munaishi katika inchi yao. Lakini mimi na jamaa yangu, tutamutumikia Yawe.”


Alipomwua yule Mufilistini Goliati, alihatarisha maisha yake, naye Yawe aliwapa Waisraeli ushindi mukubwa. Wewe ulipoona jambo lile ulifurahi. Kwa nini unataka kutenda zambi kwa kumwanga damu isiyokuwa na kosa kwa kumwua Daudi bila sababu?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ