Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 4:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Ukikaa kimya wakati kama huu, musaada utawafikia Wayuda kutoka pahali pengine, nao wataokolewa; lakini wewe utakufa, na jamaa ya baba yako itaangamia. Ni nani anayejua pengine umefanywa kuwa malkia kwa ajili ya wakati kama huu!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 4:14
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, Abrahamu akapaita pahali pale: “Yawe anajalia,” kama inavyosemwa hata leo: “Kwa mulima wa Yawe, watu wanajaliwa.”


Yawe akawapa Waisraeli kiongozi ambaye aliwakomboa kutoka kwa Waaramu. Halafu wakakaa kwa amani kama vile walivyokuwa zamani.


Nao wakamwambia Isaya: “Hezekia anasema hivi: ‘Leo ni siku ya huzuni, ya kuazibiwa na ya kuzarauliwa. Sisi tumekuwa kama mwanamuke anayetaka kuzaa mutoto, lakini hana nguvu ya kumuzaa.


Haukutuacha tuishi katika utumwa ingawa tulikuwa watumwa. Uliwafanya wafalme wa Persia wakuwe wema kwetu na kuturuhusu tuishi na kuijenga nyumba yako iliyokuwa imebomoka, na ukatufanya tukae salama hapa Yuda na Yerusalema.


Lakini mimi nikajiuliza ndani ya moyo: “Mutu kama mimi ataweza kukimbia? Mutu kama mimi anahitaji kuingia katika hekalu apate kuponyesha maisha yake? Sitaingia hata kidogo katika hekalu.”


Wakati ukafika wa Esteri kwenda kwa mufalme. Huyo, binti wa marehemu Abihaili, binamu ya Mordekayi, na ambaye alilelewa na Mordekayi, hakuomba kitu chochote zaidi ya kile alichopangiwa na Hegayi, towashi mwangalizi wa wanawake wa mufalme. Esteri akapata kukubaliwa mbele ya kila mutu aliyemwona.


Mufalme akamupenda zaidi Esteri kuliko wanawake wote. Naye Esteri akapata kukubaliwa na kutendewa mema mbele yake zaidi kuliko wabinti wengine wote. Basi, mufalme akamuvalisha taji ya kimalkia kwenye kichwa, akamufanya malkia pahali pa Vashiti.


Alikuwa anamulea binamu yake Hadasa ndiye Esteri. Esteri alikuwa binti muzuri wa sura na umbo. Wazazi wake walipokufa, Mordekayi akamutwaa Esteri, akamulea kama binti yake.


akamutumia onyo hili: “Usizani kwamba kwa sababu upo katika nyumba ya kifalme wewe uko salama zaidi kuliko Muyuda mwingine yeyote.


Haniachi hata nipumue; maisha yangu anayajaza uchungu.


wakati wa kupasua na wakati wa kushona, wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema,


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Maana mimi niko pamoja nawe, nipate kukuokoa. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote, ambayo niliyokusambaza kati yao; lakini sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakuazibu kadiri unavyostahili wala sitakuachilia uende bila kukuazibu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Usiogope, ee Yakobo mutumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo nimekutawanya kati yao, lakini wewe sitakuangamiza. Nitakuazibu kadiri unavyostahili, sitakuacha bila kukuazibu.


basi, hapo nami nitakumbuka agano langu na Abrahamu, Isaka na Yakobo na kukumbuka ile inchi niliyowaahidia.


Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.


Na kama Mungu asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya watu wake aliowachagua, yeye atazipunguza.


Yawe atawatetea watu wake, na kuwahurumia watumishi wake, wakati atakapoona nguvu zao zimeisha wala hakuna aliyebaki, mufungwa au mutu huru.


Wafilistini walipotaka kujua aliyefanya hayo, waliambiwa: “Ni huyo Samusoni, mukwe wa Mutimuna, ndiye amefanya hivyo kwa sababu huyo baba mukwe wake ametwaa muke wake na kumwoesha kwa kijana mumoja aliyekuwa rafiki ya Samusoni mwenyewe katika arusi.” Basi Wafilistini wakaenda kumuchoma kwa moto yule mwanamuke pamoja na baba yake.


Kwa heshima ya jina lake kubwa, Yawe hatawatupa watu wake kwa sababu amependa kuwafanya ninyi mukuwe watu wake.


Daudi akamujibu: “Sasa nimefanya nini? Siwezi kuuliza neno tu?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ