Mufalme akaamuru wakubwa wote wa serikali yake wamutii Hamani kwa kuinama na kupiga magoti mbele yake. Lakini Mordekayi hakuinama wala kupiga magoti mbele yake.
Kila siku walimushauria aache tabia hiyo, lakini Mordekayi hakukubaliana nao. Alikataa kufanya hivyo akisema kwamba yeye ni Muyuda na kwa hiyo hawezi kuinama mbele ya Hamani. Basi, wakamujulisha Hamani kusudi waone kama ataivumilia tabia ya Mordekayi.
Hamani akatoka kule kwenye karamu mwenye furaha tele na moyo mukunjufu. Lakini alipomwona Mordekayi kwenye mulango wa nyumba ya kifalme, hasimami wala hamupi heshima, Hamani akawaka hasira.
Kwa hiyo, mufalme Nebukadneza akawaka hasira, sura yake ikabadilika kwa chuki juu ya Sadiraki, Mesaki na Abedenego. Akaamuru kwamba moto wa furu uongezwe mara saba kuliko kawaida yake.