Esteri 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
2 Mufalme akaamuru wakubwa wote wa serikali yake wamutii Hamani kwa kuinama na kupiga magoti mbele yake. Lakini Mordekayi hakuinama wala kupiga magoti mbele yake.
Mufalme akamupandisha katika gari lake la pili na walinzi wakatangulia mbele ya Yosefu wakilalamika kwa sauti na kusema: “Mupige magoti!” Ndivyo mufalme alivyomupa Yosefu madaraka makubwa juu ya inchi yote ya Misri.
Wakati Mordekayi alipokuwa anaikaa kwenye mulango wa mufalme, Bigitani na Teresi, wawili kati ya matowashi wa mufalme waliokuwa walinzi wa milango ya vyumba vya mufalme, walikasirika hata wakafanya shauri baya la kumwua mufalme Ahasuero.
Hamani akatoka kule kwenye karamu mwenye furaha tele na moyo mukunjufu. Lakini alipomwona Mordekayi kwenye mulango wa nyumba ya kifalme, hasimami wala hamupi heshima, Hamani akawaka hasira.
Kisha Yawe akamwambia Musa: “Uandike jambo hili katika kitabu, likuwe ukumbusho. Tena umwambie Yoshua kwamba nitawafuta kabisa Waamaleki katika dunia.”
Danieli akamwomba mufalme, naye mufalme akawaweka Sadiraki, Mesaki na Abedenego kuwa wasimamizi wa mambo ya utawala ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli akabakia katika nyumba ya mufalme.
Kwa hiyo wakati Yawe, Mungu wenu, atakapowapumzisha kutokana na mashambulio ya waadui zenu wote wanaowazunguka katika inchi ambayo amewapa kuwa urizi wenu na kuishi humo, munapaswa kuangamiza Waamaleki wote.
Sasa, uende kushambulia na kuangamiza vitu vyote wanavyokuwa navyo. Usiwaache wazima, lakini uwaue wote: wanaume kwa wanawake, watoto wachanga na wenye kunyonya, ngombe, kondoo, ngamia na punda.’ ”