Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 3:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Wajumbe wakazipeleka barua hizo kwa kila jimbo katika utawala ule. Tangazo hilo lilisema kwamba kwa siku moja tu, ni kusema siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili unaoitwa Adari, Wayuda wote – tangia kwa vijana mpaka wazee, wanawake na watoto, wote wauawe, waangamizwe na kuteketezwa kabisa, na mali zao zote zinyanganywe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 3:13
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo wajumbe wakapita katika inchi yote ya Israeli na ya Yuda kwa kupeleka barua zile kufuatana na amri ya mufalme na wakubwa wake. Barua hizo zilikuwa na ujumbe huu: “Enyi watu wa Israeli muliobaki nyuma ya mashambulizi ya wafalme wa Asuria. Mumurudilie Yawe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Israeli, kusudi naye apate kuwarudilia.


Maana, mimi na watu wangu tumeuzishwa kusudi tuuawe, tuangamizwe na kuteketezwa kabisa. Kama tungeuzishwa tu kuwa watumwa na wajakazi, ningekaa kimya wala nisingekusumbua. Ingawa tutateswa hakuna adui atakayeweza kulipa hasara hii kwa mufalme.”


“Ikikupendeza, ewe mufalme, na kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ukiona ni vizuri nami nikikupendeza, tafazali, toa tangazo la kuvunja mipango ambayo Hamani alikuwa ameamuru itimizwe. Mipango hiyo ni ile ya mwana wa Hamedata, wa uzao wa Agagi, aliyopanga kwa kuwaangamiza Wayuda wote katika majimbo yote.


Siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, ni kusema mwezi wa Adari, ilipofika, siku ambayo tangazo la mufalme lingetimizwa, na waadui za Wayuda walitarajia kuwashinda Wayuda, ikageuzwa kuwa siku ya ushindi kwa Wayuda juu ya waadui zao.


wana kumi wa Hamani mwana wa Hamedata, adui ya Wayuda. Hata hivyo, hawakunyanganya mali zao.


Basi, Wayuda wakawashambulia waadui zao kwa upanga, wakawachinja, wakawaangamiza na kuwatendea kama walivyopenda.


Siku zangu zinaenda mbio kuliko mukimbiaji, zinakimbia bila kuona faida.


Nilimutuma kuliazibu taifa ovu, nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia, kuwanyanganya na kuteka vitu vyao, na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.


Wakimbiaji wanakimbia wakitoleana ujumbe mumoja kwa mwingine kwa kumupasha mufalme wa Babeli habari kwamba muji wake umeshambuliwa kila upande.


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Sasa, uende kushambulia na kuangamiza vitu vyote wanavyokuwa navyo. Usiwaache wazima, lakini uwaue wote: wanaume kwa wanawake, watoto wachanga na wenye kunyonya, ngombe, kondoo, ngamia na punda.’ ”


Kisha aliwaua kwa makali ya upanga wakaaji wote wa Noba, muji wa makuhani, wanaume na wanawake, watoto wadogo na wenye kunyonya, ngombe, punda na kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ