Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 3:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Basi, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kwanza, Hamani akawaita waandishi wote wa mufalme, akawapa tangazo ambalo alitaka litafsiriwe kwa kila luga na kila namna ya maandiko katika utawala ule, na halafu mifano ya barua isambazwe kwa watawala wote, wakubwa wa majimbo yote, na viongozi wa makabila – kufuatana na luga zinazotumika kwao. Tangazo hilo likatolewa kwa jina la mufalme Ahasuero, na kupigwa muhuri kwa pete yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 3:12
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yezebeli akaandika barua kwa jina la Ahabu na kuzipiga muhuri wa mufalme. Kisha akapeleka barua hizo kwa wazee na watu wenye heshima walioishi na Naboti kule katika muji.


Vilevile wakawapa wasimamizi wa mufalme na watawala wa mukoa wa majimbo ya upande wa magaribi wa muto Furati maagizo waliyopewa na mufalme, nao wakatoa musaada kwa watu na kwa ajili ya nyumba ya Mungu.


Basi, akapeleka barua kwa kila jimbo kwa luga na maandiko yanayoeleweka katika jimbo: kwamba kila mwanaume akuwe bwana wa nyumba yake, na kuitangaza habari hii kwa luga yake.


Halafu mufalme akamwambia Hamani: “Umepewa watu wote na feza zile, tumia vile unavyopenda.”


Mufalme akaivua pete yake ya muhuri aliyokuwa amemunyanganya Hamani, akamupa Mordekayi. Esteri naye akamupa Mordekayi mamlaka juu ya mali ya Hamani.


Wayuda wakaifanya kuwa sheria kwao, kwa wazao wao na kwa mutu yeyote ambaye angejiunga nao, kwamba katika wakati uliopangwa kila mwaka, bila kukosa, siku hizo mbili zishikwe kulingana na maagizo ya Mordekayi.


Wewe, ee mufalme, ulitoa amri kwamba kila mutu anaposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na kila aina ya muziki, ainame chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu.


Watu wale waliofanya mupango mubaya juu ya Danieli waliingia ndani, wakamukuta Danieli akiomba na kumusihi Mungu wake.


Mufalme aliposikia maneno hayo, alisikitika sana. Akafanya nguvu yake yote kwa kutafuta njia ya kumwokoa Danieli. Aliendelea kujaribu mpaka jua likatua.


Mufalme akaamuru wale watu waliomuchongea Danieli wakamatwe, nao wakatupwa ndani ya lile pango la simba pamoja na wake wao na watoto wao. Nao, hata mbele hawajagusa chini, simba waliwashambulia na kuivunjavunja mifupa yao.


Sisi wakubwa uliotuweka, wasimamizi, maliwali, washauri na wakubwa wa majimbo, wote tumepatana kwamba inafaa, ee mufalme, utoe amri na kuhakikisha kwamba inafuatwa kikamilifu. Amuru kwamba kwa muda wa siku makumi tatu kusikuwe mutu yeyote atakayeruhusiwa kuomba kitu chochote kwa mungu yeyote au kwa mutu yeyote, isipokuwa kutoka kwako wewe, ewe mufalme. Mutu yeyote atakayevunja sheria hii atupwe katika pango la simba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ