Wewe ndiwe utakayeisimamia inchi yangu, na watu wangu wote watakuwa chini ya amri yako. Mimi tu ndiye mukubwa kuliko wewe kwa kuwa ninaikalia kiti cha kifalme.
Mimi pamoja na washauri wangu saba, tunakutuma uende ufanye uchunguzi kule Yuda na Yerusalema kuona kama Sheria ya Mungu wako ambayo umepewa inafuatwa kikamilifu.
Washauri wake wa kawaida walikuwa Karsena, Setari, Adimata, Tarsisi, Maresi, Marsena na Memukani – viongozi saba wa Persia na Media waliokuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.
Halafu akaanza kueleza juu ya utajiri anaokuwa nao, wana anaokuwa nao, jinsi mufalme alivyomupandisha cheo, na jinsi alivyopewa madaraka zaidi kuliko wakubwa wengine wote wa mufalme.
Kisha Esteri akazungumuza tena na mufalme; akajitupa chini, kwenye miguu ya mufalme, naye akilia, akamusihi mufalme aukomeshe mupango mubaya ambao Hamani, wa uzao wa Agagi, alikuwa amepanga juu ya Wayuda.
Samweli akasema: “Kwa sababu upanga wako umewafanya wamama wengi wasikuwe na watoto, ndivyo na mama yako atakavyokuwa bila mutoto kati ya wamama.” Akamukatakata Agagi vipandevipande mbele ya Yawe kule Gilgali.