Harbona, mumoja wa wale matowashi waliomutumikia mufalme, akasema: “Hamani amesubutu hata kutengeneza muti wa kumutundikia Mordekayi ambaye aliyaokoa maisha yako, ewe mufalme. Muti huo, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili, bado uko kule katika nyumba yake.” Hapo mufalme akaamuru: “Mumutundike Hamani juu ya muti uleule.”