Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 2:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Wakati Mordekayi alipokuwa anaikaa kwenye mulango wa mufalme, Bigitani na Teresi, wawili kati ya matowashi wa mufalme waliokuwa walinzi wa milango ya vyumba vya mufalme, walikasirika hata wakafanya shauri baya la kumwua mufalme Ahasuero.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 2:21
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tena mufalme Daudi akamwambia Abisayi na hata watumishi wake wote: “Ikiwa mutoto wangu mwenyewe anayawinda maisha yangu, si ni zaidi kwa mutu wa kabila la Benjamina? Ninyi muache anilaani maana Yawe amemwagiza anilaani.


Jemadari wake Simuri ambaye alisimamia nusu ya kundi ya magari yake ya vita alimwasi. Siku moja, mufalme Ela alipokuwa kule Tirza katika nyumba ya Arsa aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, alikunywa, akalewa.


Mambo mengine ya Yoasi na yote aliyofanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.


Kisha watumishi wa Amoni walimwasi na kumwua katika nyumba yake ya kifalme.


Kwa mwanzo wa utawala wa mufalme Ahasuero, waadui za watu waliokaa Yuda na Yerusalema wakaandika mashitaki juu yao.


Wabinti walipokusanyika mara ya pili, Mordekayi alikuwa anaikaa kwenye mulango wa mufalme.


Usiku ule, mufalme hakupata usingizi. Basi, akaamuru kitabu cha Mambo ya Siku cha matukio ya kila siku, kiletwe, nacho kikasomwa mbele yake.


Ikaonekana jinsi ilivyoandikwa ikielezwa jinsi Mordekayi alivyopasha habari ya shauri la kumwua mufalme iliyokuwa imefanywa na Bigitani na Teresi, hao wawili kati ya matowashi wa mufalme waliokuwa walinzi wa vyumba vya mufalme.


wewe unayewapa wafalme ushindi, unayemwokoa mutumishi wako Daudi!


Danieli akamwomba mufalme, naye mufalme akawaweka Sadiraki, Mesaki na Abedenego kuwa wasimamizi wa mambo ya utawala ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli akabakia katika nyumba ya mufalme.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ