Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 2:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Kisha mufalme akafanya karamu kubwa kwa heshima ya Esteri, akawaalika viongozi na watumishi wote wa serikali yake. Vilevile, mufalme akatangaza musamaha wa kodi katika majimbo yote, akatoa zawadi nyingi kulingana na mapato yake ya kifalme.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 2:18
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Labani akafanya karamu na kuwaalika watu wote wa kule.


Halafu, Walawi wakawatuliza watu wote, wakisema: “Munyamaze maana siku ya leo ni takatifu; musihuzunike.”


Watu walipewa vinywaji katika vikombe mbalimbali vya zahabu. Na divai ya kifalme ilikuwa nyingi sawa mapato ya mufalme.


Wayuda walishinda waadui zao katika siku hizo, na katika mwezi huo huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha, na kilio chao kuwa sikukuu. Waliagizwa wakuwe wanazikumbuka siku hizo kwa kufanya karamu na sherehe, kupelekeana zawadi za chakula na kuwapa wamasikini vitu.


Mukuje basi enyi wabinti wa Sayuni, mumwone mufalme Solomono. Amevaa taji aliyovalishwa na mama yake, siku alipofanya ndoa yake, siku ambayo moyo wake ulijaa furaha.


Ninaingia katika bustani yangu, dada yangu, muchumba wangu. Ninakusanya manemane na majani yenye harufu, ninakula sega langu la asali, ninakunywa divai yangu na maziwa yangu. Mukule, enyi warafiki, mukunywe; mukunywe sana, wapendwa wangu.


“Ufalme wa mbinguni unafanana na mufalme mumoja aliyemufanyia mwana wake karamu ya ndoa.


Siku moja Herodia alipata wakati wa kumwua Yoane. Ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, wakati alipofanya karamu kwa wasimamizi wa serikali yake, wakubwa wa waaskari na waheshimiwa wa Galilaya.


“Wakati mutu anapokualika kwa karamu ya ndoa, usiikae kwenye viti vya mbele. Labda kati ya waalikwa kuna mutu mwenye heshima kukupita.


Wakaaji wa dunia watafurahi kwa ajili ya kifo chao na kushangilia. Watatumiana zawadi, kwa maana manabii hawa wawili waliwasumbua sana wakaaji wa dunia.


Halafu malaika akaniambia: “Andika maneno haya: Heri wale wanaoalikwa kwa karamu ya ndoa ya Mwana-Kondoo.” Naye akasema tena: “Maneno haya ni ya kweli yanayotoka kwa Mungu.”


Ukiwauliza, watakuambia. Sasa ninakuomba vijana wangu hawa wapate kukubaliwa mbele yako, maana tumefika wakati wa sikukuu. Tafazali uwapatie kitu chochote unachokuwa nacho watumishi wako hawa nami mwana wako Daudi.’ ”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ