Kisha mufalme akarudi kutoka katika bustani, na mara alipoingia ndani ya chumba walimokuwa wanakunywa divai, akamukuta Hamani amejitupa karibu na kiti ambamo Esteri alikuwa ameikaa. Kuona hivyo, mufalme akasema kwa sauti kubwa: “Hivi mutu huyu anataka kumushika kwa nguvu malkia mbele yangu, tena ndani ya nyumba ya kifalme?” Mara tu mbele mufalme hajamaliza kusema, matowashi wakamufunika Hamani uso.