Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Esteri 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Basi, kwa muda wa miezi sita, Ahasuero akaonyesha utajiri wa ufalme wake mutukufu, na sifa ya utawala wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Esteri 1:4
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamupa Solomono sifa nzuri mbele ya Waisraeli wote, akamupa utukufu wa kifalme unaopita utukufu wa mufalme yeyote aliyeitawala inchi ya Israeli mbele yake.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, mufalme Ahasuero akaandaa karamu kwa ajili ya viongozi na watumishi wake wa serikali, wakubwa wa majeshi ya Persia na Media, watu wenye heshima na wakubwa wa majimbo.


Muda ule ulipomalizika, mufalme aliandaa karamu kwa ajili ya watu wote wa muji mukubwa wa Susani, wakubwa kwa wadogo. Karamu hiyo iliyokamata muda wa siku saba, ilifanyika ndani ya kiwanja, katika bustani ya nyumba ya kifalme.


Basi, ujionyeshe kuwa na utukufu na ukubwa, ujipambe kwa heshima na mamlaka.


Nitasema juu ya utukufu na mamlaka yako, nitafikiri juu ya matendo yako ya ajabu.


Alikuomba maisha, nawe ukamupatia; ulimupatia siku nyingi milele na milele.


Wewe ni muzuri kuliko wanadamu wote, maneno yako ni rehema tupu, Mungu amekubariki milele.


Yawe anatawala; amejifunika utukufu mukubwa! Yawe amevaa utukufu na nguvu! Ameimarisha ulimwengu, hautatikisika hata kidogo.


Basi, Hezekia aliwakaribisha na kuwaonyesha nyumba alimoweka mali yake: feza, zahabu, viungo vya kukoleza chakula, mafuta ya bei kali, vifaa vyake vyote vya vita na vitu vyote vilivyokuwa katika gala zake. Hakuna chochote katika nyumba yake ya kifalme au katika inchi yake ambacho hakuwaonyesha.


Kwa werevu wako mukubwa katika biashara umejiongezea utajiri wako, ukakuwa na kiburi kwa ajili ya mali zako!


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Ee mufalme, Mungu Mukubwa alimupa baba yako mufalme Nebukadneza ufalme, ukubwa, mamlaka na utukufu.


Shetani akamupeleka tena mpaka juu ya mulima murefu, akamwonyesha falme zote za dunia na utajiri wao.


Usituache kuanguka katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. [Kwa maana ufalme, uwezo na utukufu ni vyako hata milele. Amina.]’


Vilevile alitaka kuonyesha uwingi wa utukufu wake kwa wale aliowasikilia huruma; wale ambao alitayarisha tangu zamani kwa kuwatukuzisha.


Ninaomba Mungu aifungue mioyo yenu ipate kuona mwangaza wake. Kwa hiyo mutapata kujua tumaini munalokuwa nalo kutokana na mwito wa Mungu. Vilevile mupate kujua utajiri mukubwa wa urizi anaouwekea watu wake,


Kwa maana Mungu alitaka kuwafunulia watu hao siri ya mupango wake wenye utajiri mukubwa alioufanya kwa ajili ya mataifa yote. Nayo siri ile ni kwamba Kristo ni ndani yenu, naye ndiye anayetuletea tumaini kwamba tutashiriki katika utukufu wa Mungu.


“Bwana wetu na Mungu wetu, wewe unastahili utukufu, heshima na uwezo, kwa maana wewe ndiwe uliyeumba vitu vyote; vile vimeumbwa na kupata kuwa kutokana na mapenzi yako.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ