Esteri 1:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
18 Leo hii, wanawake wa Persia na Media ambao wamesikia jinsi malkia Vashiti alivyofanya, watakuwa wanawaelezea viongozi wako; hivyo mazarau na chuki vitajaa kila pahali.
Tendo hili la malkia Vashiti litajulikana na wanawake wote, nao watawazarau waume zao, wakisema: ‘Mufalme Ahasuero aliamuru malkia Vashiti akuje kwake, lakini yeye akakataa.’
Basi, ikikupendeza, ewe mufalme, toa amri kwamba Vashiti asikuje tena mbele yako. Amri hiyo iandikwe katika sheria za Persia na Media, kusudi isiweze kubadilishwa. Kisha, cheo chake cha umalkia, kipewe kwa mwanamuke mwingine anayekuwa bora zaidi kuliko yeye.