Esteri 1:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
16 Hapo Memukani akamwambia mufalme na viongozi wake: “Zaidi ya kumukosea mufalme, malkia Vashiti amewakosea viongozi na kila mutu katika majimbo ya mufalme Ahasuero!
Tendo hili la malkia Vashiti litajulikana na wanawake wote, nao watawazarau waume zao, wakisema: ‘Mufalme Ahasuero aliamuru malkia Vashiti akuje kwake, lakini yeye akakataa.’
Paulo alipotaka kusema, Galio akawaambia Wayuda: “Kama mungemushitaki mutu huyu juu ya neno la uovu au kosa kubwa alilofanya, ningewasikiliza ninyi Wayuda vema.
Paulo akajibu: “Mimi ninasimama mbele ya tribinali ya Mufalme wa Roma, na ni hapa ninapopaswa kusambishwa. Sikuwakosea Wayuda kosa lolote, kama vile wewe mwenyewe unavyojua vizuri.