Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 9:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Ee Bwana, sisi tumefezeheka, wafalme wetu, wakubwa wetu na babu zetu, kwa sababu tumekutendea zambi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 9:8
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitawatendea hayo yote kwa sababu wameniasi na kunikasirikisha tangia wakati wazee wao walipotoka Misri mpaka leo.”


kama watakapokuwa kule katika uhamisho watajifikiri kwa roho yao yote na kwa moyo wao wote na kutubu na kukuomba musamaha, wakisema: ‘Tumetenda zambi; tumepotoka na kufanya maovu’,


Usikilize kwa uangalifu maombi yangu, na uniangalie mimi mutumishi wako, ninapokuomba kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli, usiku na muchana. Ninaungama zambi za watu wa Israeli, tulizofanya mbele yako. Mimi pamoja na watu wa jamaa yangu tumefanya zambi.


Wewe unakuja kuwasaidia wanaotenda haki kwa furaha, wanaokukumbuka na kufuata njia zako. Ulitukasirikia tulipokuwa wenye zambi; sisi tumeasi kwa muda murefu.


Tunakubali uovu wetu, ee Yawe, tunakubali uovu wa babu zetu, maana, tumekukosea wewe.


kwa sababu ya uovu wote watu wa Israeli na Wayuda waliotenda, pamoja na wafalme na wakubwa wao, makuhani na manabii wao, na wakaaji wa Yerusalema.


Lakini ni nani wanayemukasirikisha? Mimi? Hata kidogo! Wanajikasirikisha wao wenyewe na kujifezehesha! –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini Yawe amefanya sawa kwa maana nimeliasi neno lake. Munisikilize enyi watu wote, muyaangalie mateso yangu. Wabinti zangu na vijana wangu wanaume wamepelekwa katika utumwa.


Tulikukosea na kukuasi, nawe haujatusamehe bado.


Taji tuliojivunia imeanguka. Ole kwetu maana tumetenda zambi!


Nitakusamehe kila kitu ulichotenda. Nawe utakapokumbuka hayo yote uliyotenda utashangaa na kunyamaza kwa sababu ya haya wala hautasubutu kusema tena. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Lakini wakaaji wake wameyaasi maagizo na masharti yangu, wakakuwa wabaya kuliko mataifa na inchi zinazowazunguka. Kweli, wameyakataa maagizo yangu na kuacha kuyafuata masharti yangu.


Wewe, Bwana Mungu wetu, una huruma na musamaha, ingawa sisi tumekuasi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ