Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 9:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kwako, ee Bwana, kuna haki, lakini sisi tumepata haya siku zote. Jambo hili ni kweli kwetu sisi wote tunaoishi Yudea, wakaaji wa muji Yerusalema na Waisraeli wote ambao umewatawanya katika inchi za mbali na za karibu kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 9:7
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata nyuma ya yote yaliyotupata kwa sababu ya maovu yetu na makosa yetu mengi, tunajua kwamba azabu uliyotupa, ee Mungu wetu, ni ndogo ikilinganishwa na makosa yetu, na umewaacha wazima wamoja kati yetu.


Ee Yawe, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki na umetuacha tubaki kama vile tunavyokuwa hivi leo. Tunaungama makosa yetu mbele yako, tukijua kwamba hakuna anayekuwa na haki yoyote ya kuja mbele yako kwa ajili ya makosa haya.”


Hata hivyo, una haki kwa kutuazibu hivyo; maana wewe umekuwa mwaminifu wakati sisi tumekuwa watenda maovu.


Ee Yawe, wewe ni wa haki; na hukumu zako ni za usawa.


Umetufanya tuzarauliwe na watu wa mataifa; wanatutikisia vichwa vyao kwa kutusimanga.


Unirudishie furaha ya wokovu wako, uniimarishe kwa Roho wako mwema.


Unisafishe kabisa kosa langu; unitakase zambi yangu.


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


Watengenezaji wa sanamu watapata haya na kuzarauliwa, wote pamoja watafezeheka.


Ee Yawe, wewe ni mwenye haki, ingawa nitakushitaki. Lakini ningependa nibishane nawe juu ya mambo ya haki: Kwa nini waovu wanafanikiwa katika mambo yao? Mbona wote wanaodanganya wanastawi?


Katika siku za utawala wake, inchi ya Yuda itaokolewa na inchi ya Israeli itakuwa katika usalama. Naye ataitwa kwa jina la Yawe Ni Haki Yetu.


Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza mbele ya falme zote za dunia. Watakuwa kitu cha zihaka, kitu cha kuzomewa, kuchekelewa na kulaaniwa kila fasi nitakapowasambaza.


Sherti tujilaze chini kwa ajili ya haya, na kujiachilia kufunikiwa na haya yetu. Tangu ujana wetu mpaka leo hii, sisi wenyewe, kama vile babu zetu, tumetenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wetu, wala hatukumutii Yawe, Mungu wetu.


kwa sababu ya uovu wote watu wa Israeli na Wayuda waliotenda, pamoja na wafalme na wakubwa wao, makuhani na manabii wao, na wakaaji wa Yerusalema.


Wakati huo inchi ya Yuda itaokolewa na Yerusalema utakuwa salama. Na muji huo utaitwa “Yawe ni Ukombozi Wetu”.


wanauzunguka Yerusalema kama walinzi wanavyozunguka mashamba, kwa sababu watu wake wameniasi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini ni nani wanayemukasirikisha? Mimi? Hata kidogo! Wanajikasirikisha wao wenyewe na kujifezehesha! –Ni ujumbe wa Yawe.


Nitakusamehe kila kitu ulichotenda. Nawe utakapokumbuka hayo yote uliyotenda utashangaa na kunyamaza kwa sababu ya haya wala hautasubutu kusema tena. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Kisha mutakapokumbuka mienendo yenu miovu na matendo yenu mabaya, mutajichukia wenyewe kwa sababu ya maovu yenu na machukizo muliyofanya.


Hukohuko katika muji wazazi watawakula watoto wao wenyewe na watoto watawakula wazazi wao. Nitatimiza hukumu zangu juu yenu na watakaobaki wazima nitawasambaza pande zote.


Anayekuwa mbali sana atakufa kwa ugonjwa mukali. Anayekuwa karibu atauawa kwa upanga. Atakayekuwa amebaki na kuponyoka hayo mawili atakufa kwa njaa. Ndivyo nitakavyotimiza kasirani yangu juu yao.


Kwa hiyo, ee Yawe, Mungu wetu, ulikuwa tayari kutuazibu, na ukafanya hivyo, kwa sababu unafanya mambo yanayokuwa ya haki, nasi hatukukusikiliza.


Tega sikio, ee Mungu wangu; angalia uone taabu tunazokuwa nazo na jinsi huo muji unaoitwa kwa jina lako unavyotaabika. Tunakutolea maombi yetu si kwa sababu tumetenda haki, lakini kwa sababu wewe una huruma nyingi.


Ee Bwana, sisi tumefezeheka, wafalme wetu, wakubwa wetu na babu zetu, kwa sababu tumekutendea zambi.


Nitatoa amri, na kuwapepeta Waisraeli kati ya mataifa kama mutu anavyopepeta ngano kusudi niwatoshe wote wasiofaa.


Basi mulipata faida gani kwa kufanya mambo yale munayopata haya juu yake sasa? Maana mwisho yao ni kifo!


Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.


Yawe atawatawanya kati ya mataifa mengine, na ni wachache tu wenu watakaobakia huko ambako Yawe atawafukuzia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ