kwa sababu Waisraeli hawakutii sauti ya Yawe, Mungu wao, lakini walivunja agano lake, hata hawakusikia wala kutii yote Musa, mutumishi wa Yawe, aliyowaamuru.
nikisema: “Ee Mungu wangu, ninaona haya kubwa sana kukiinua kichwa changu mbele yako. Zambi zetu zimelundikana kupita hata vichwa vyetu; makosa yetu yanafika hata mbinguni.
Tumekuasi na kukukana, ee Yawe, tumekataa kukufuata, ewe Mungu wetu. Tunasema maneno ya kutesa na uasi, katika mioyo yetu tunatunga na kutoa maneno ya uongo.
Wewe unakuja kuwasaidia wanaotenda haki kwa furaha, wanaokukumbuka na kufuata njia zako. Ulitukasirikia tulipokuwa wenye zambi; sisi tumeasi kwa muda murefu.
Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.
Sherti tujilaze chini kwa ajili ya haya, na kujiachilia kufunikiwa na haya yetu. Tangu ujana wetu mpaka leo hii, sisi wenyewe, kama vile babu zetu, tumetenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wetu, wala hatukumutii Yawe, Mungu wetu.
Wapenzi wako wote wamekusahau; hawajali kitu chochote juu yako. Nimekupiga sawa vile ungekuwa adui yangu. Umeazibiwa bila huruma, kwa sababu kosa lako ni kubwa, zambi zako ni nyingi sana.
Imekuwa hivyo kwa sababu ya uovu walioufanya, wakanikasirikisha kwa kuifukizia ubani na kuitumikia miungu mingine ambayo wao wenyewe hawakuifahamu, wala ninyi, wala babu zenu.
Lakini Yawe amefanya sawa kwa maana nimeliasi neno lake. Munisikilize enyi watu wote, muyaangalie mateso yangu. Wabinti zangu na vijana wangu wanaume wamepelekwa katika utumwa.
Ona, ee Yawe, ninavyokuwa tabani. Roho yangu imechafuka, moyo wangu unaugua maana nimekuasi vibaya. Kule inje kumejaa mauaji, ndani nako ni kama kifo tu.
Lakini wakaaji wake wameyaasi maagizo na masharti yangu, wakakuwa wabaya kuliko mataifa na inchi zinazowazunguka. Kweli, wameyakataa maagizo yangu na kuacha kuyafuata masharti yangu.
Halafu wale walioponyoka watanikumbuka katikati ya mataifa ambamo watakuwa wamepelekwa katika uhamisho. Nitakuwa nimewavunja moyo wao wa uzinzi ambao ulinitupilia mbali, na macho yao yaliyozini na sanamu zao. Kwa hiyo watajichukia wao wenyewe kwa sababu ya maovu na machukizo yao yote waliyoyatenda.
Waisraeli wote wameiasi sheria yako, wamekuacha wakakataa kukutii. Kwa sababu tumekukosea, tumemwangiwa laana na viapo vilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, mutumishi wako.
Na sasa ee Bwana, Mungu wetu, uliyewaondoa watu wako katika inchi ya Misri kwa nguvu yako kubwa na kulifanya jina lako litukuzwe mpaka sasa, tunasema kwamba tumetenda zambi; tumefanya maovu.
Yawe alipoanza kusema na Waisraeli kwa njia ya Hosea, alimwambia hivi: Kwenda kuoa mwanamuke muzinzi, uzae naye watoto wa uzinzi, maana watu wa inchi hii wanafanya uzinzi mwingi kwa kuniacha mimi.
Tangu wakati wa babu zenu, mumeyazarau masharti yangu wala hamukuyafuata. Munirudilie, nami nitawageukia. Lakini ninyi munaniuliza: Tutakurudilia namna gani?
Basi wandugu zangu, muangalie vizuri, kati yenu kusikuwe mutu mumoja mwenye moyo mubaya wa kutokuamini, aliyefikia hata kujitenga mbali na Mungu Mwenye Uzima.