Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 9:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Nilimwomba Yawe, Mungu wangu, na kuitikia zambi, nikisema: Ee Bwana, wewe ni Mungu mukubwa na wa kuogopesha. Wewe unashika agano lako na kutenda mema kwa wanaokupenda na kuzitii amri zako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 9:4
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

akasema: “Ee Yawe, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu mwingine kama wewe, juu mbinguni, au chini katika dunia. Wewe unashika agano lako na kutenda wema kwa watumishi wako wanaoishi wakikutii kwa moyo wao wote.


kama watu wangu hao wakijinyenyekeza, wakiomba, wakinitafuta na kuacha njia zao mbaya, basi, mimi nitawasikiliza kutokea juu mbinguni, nitawasamehe zambi yao na kustawisha inchi yao.


Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama naye akilia na kujiangusha uso mpaka chini mbele ya nyumba ya Mungu, kundi kubwa la watu wa Israeli, wanaume, wanawake na watoto, wakakusanyika karibu naye wakilia kwa uchungu mwingi.


nikisema: “Ee Yawe, Mungu wa mbinguni, wewe ni Mungu unayekuwa mukubwa na wa kutisha, unashika agano lako na kutenda mema kwa wale wanaokupenda na kushika amri zako.


Kwa hiyo, ee Mungu wetu, Mungu mukubwa, mwenye nguvu na wa kutisha, wewe unashika agano lako na kutenda wema. Mateso yaliyotupata, sisi, wafalme wetu, wakubwa wetu, makuhani wetu, manabii wetu, babu zetu na watu wako wote tangu wakati wa wafalme wa Asuria mpaka leo, usiyaone kuwa ni madogo.


Kisha niliitikia makosa yangu mbele yako, wala sikuficha uovu wangu. Nilisema kwamba nitaungama makosa yangu mbele ya Yawe. Nawe ukanisamehe zambi yangu.


Lakini ninawatendea mema maelfu ya wale wanaonipenda na kushika amri zangu.


Wewe, kubali tu kosa lako: kwamba umeniasi mimi Yawe, Mungu wako; kwamba chini ya kila muti wenye majani, umeonyesha mapenzi yako kwa miungu mingine, wala haukuitii sauti yangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.


Hivyo, mufalme Dario akatia sahihi kwenye sheria hiyo.


Nilimwomba Yawe, kwa moyo, nikimutolea maombi pamoja na kufunga kula chakula, nikavaa gunia na kuikaa kwenye majivu.


Aliahidi kuwasikilia babu zetu huruma; na kukumbuka agano lake takatifu,


Tunajua kwamba katika mambo yote Mungu anatumika kwa kuwajalia wale wanaomupenda, ndio wale walioitwa naye kufuatana na kusudi lake.


Lakini ninawatendea mema maelfu ya wale wanaonipenda na kushika amri zangu.


“Mukisikiliza maagizo haya na kuyashika hata kuyatenda, Yawe, Mungu wenu, atashika agano lake nanyi na kuwatendea mema kama vile alivyowaahidi babu zenu.


Basi, musiwaogope, kwa sababu Yawe, Mungu wenu, yuko kati yenu. Yeye ni Mungu mukubwa na wa kutisha.


Basi, mujue kwamba Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu. Yeye ni Mungu mwaminifu, anayeshika agano lake na kutenda mema kwa vizazi vingi vya wale wanaomupenda na kushika amri zake.


Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.


Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ