Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 9:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Kisha majuma hayo makumi saba na mawili, yule aliyepakwa mafuta atauawa na hatabaki na kitu. Muji na Pahali Patakatifu Sana vitaharibishwa na waaskari wa mutawala atakayekuja kushambulia. Mwisho wake utafika kama mafuriko, kukiwa vita na maangamizi kama yalivyopangwa na Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 9:26
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wao wakamwambia mufalme: “Saulo alikusudia kutuua sisi na kutuangamiza kusipate kubakia mutu yeyote wetu popote katika eneo lolote la Israeli.


Nimekwisha kama maji yaliyomwangika; mifupa yangu yote imeteguka; moyo wangu ni kama inta, unayeyuka ndani yangu.


Bwana amejichagulia mutu wake shujaa na mwenye nguvu, ambaye ni kama mvua ya mawe na zoruba kali, kama zoruba ya mafuriko makubwa; kwa mukono wake atawatupa chini.


Basi, ninyi musikuwe na mazarau vifungo vyenu visipate kukazwa zaidi. Maana nimesikia kwamba Yawe wa majeshi amekusudia kuiangamiza inchi yote.


Alikamatwa kwa kinguvu, akahukumiwa na kupelekwa kuuawa; na hakuna mutu aliyejali mambo yanayomupata. Alifukuzwa kutoka inchi ya wanaokuwa wazima, kwa sababu ya makosa ya watu wangu.


basi, Bwana wao atawaletea mafuriko makubwa ya maji ya muto Furati, ni kusema mufalme wa Asuria na nguvu zake zote; yatafurika na kupita kingo zake.


Nani huyo anayekuwa kama muto Nili uliofurika, kama mito inayovumisha mawimbi?


Bahari imefurika juu ya Babeli, Babeli imefunikwa na mawimbi yaliyochafuka.


Wana wa mufalme wa kaskazini watakusanya kundi kubwa la waaskari na kujitayarisha kwa vita. Kundi hilo litasonga mbele kama mafuriko ya maji litapita na kupigana vita mpaka ndani ya muji wenye kuta wa waadui.


Huyo mushambulizi atakusudia kuja na kundi lake lote la waaskari, naye atafanya mapatano na kuyatimiza. Atamuoesha binti yake mumoja kusudi apate kuuangamiza ufalme wa adui yake; lakini mupango wake hautawezekana, wala kumufaidia kwa jambo lolote.


Makundi ya waaskari pamoja na kuhani wa hekalu wataangamizwa na kuwaua.


Mufalme atafanya kama anavyopenda. Atajitukuza na kujivuna kwamba yeye ni mukubwa kuliko miungu yote, na kumutukana Mungu wa miungu. Ataendelea kufanikiwa mpaka kasirani ifikie ukomo wake, maana yaliyopangwa sherti yatimie.


Mutawala huyo atafanya mapatano imara na watu wengi kwa muda wa miaka saba. Kisha nusu ya muda huo atakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Pahali pa juu katika hekalu patasimamishwa chukizo linaloleta uharibifu, nalo litabaki pale mpaka yule aliyemusimamisha atakapoangamizwa kama ilivyopangwa na Mungu.


Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Si wangu”, maana ninyi si watu wangu, wala mimi si Mungu wenu.


Kwa hiyo, dunia itatetemeka na kila mutu katika inchi atafanya kilio. Inchi yote itayumbayumba; itapanda na kushuka, kama vile maji ya muto Nili yanavyojaa na kupunguka!


Bwana wetu Yawe wa majeshi, anaigusa dunia nayo inatetemeka, na wakaaji wake wanaomboleza; dunia nzima inapanda na kushuka kama vile muto Nili wa Misri unavyojaa na kupunguka.


Waadui wakishambulia inchi kama mafuriko, yeye anawaangamiza; anawafuatilia na kuwafukuza mpaka katika giza.


“Ufalme wa mbinguni unafanana na mufalme mumoja aliyemufanyia mwana wake karamu ya ndoa.


Halafu mufalme akakasirika. Akawatuma waaskari wake kuwaua wale wauaji na kuteketeza muji wao kwa moto.


Lakini Yesu akawaambia: “Munaona haya yote? Kweli ninawaambia: hapa hakutabaki hata jiwe moja juu ya lingine; yote yatabomolewa.”


Yesu akamujibu: “Unaona majengo haya makubwa? Hakutabaki hata jiwe moja juu ya lingine; yote yatabomolewa.”


Mutakaposikia habari za matokeo au utetezi wa vita musiogope. Sherti mambo hayo yatukie, lakini hayaonyeshi kama mwisho umefika.


Yesu akawajibu: “Hakika Elia anapaswa kurudi kwanza kutengeneza mambo yote. Lakini sababu gani Maandiko Matakatifu yanasema vilevile kwamba Mwana wa Mutu atateswa sana na kuzarauliwa?


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


“Kutakuwa siku vitu hivi munavyoona vitabomolewa, wala hakutabaki hata jiwe moja juu ya lingine.”


Haikumupasa Kristo ateswe kama vile na aingie kwenye nafasi atakapotukuzwa?”


akiwaambia: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Kristo atateswa na kufufuka kwa siku ya tatu kisha kufa kwake.


Sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa sababu mutawala wa dunia hii anakuja. Yeye hana uwezo juu yangu,


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


Ni kwa ajili ya shabaha hiyo Mungu aliwaita kumufuata, kwa sababu Kristo vilevile aliteswa kwa ajili yenu, akiwaachia mufano, kusudi mufuate njia yake.


Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ