Danieli 9:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
23 Ulipoanza kuomba, Mungu alitoa jibu, nami nimekuja kukuelezea jibu hilo kwa sababu unapendwa sana. Kwa hiyo, usikilize kwa uangalifu jibu hilo na kuelewa maono hayo.
Kisha Isaya mwana wa Amozi akatuma ujumbe kwa Hezekia, akisema: “Yawe, Mungu wa Israeli anasema hivi: Nimesikia ombi lako kwangu juu ya Saniharibu mufalme wa Asuria.
Hata kama Noa, Danieli na Yobu wangalikuwa ndani ya inchi ile, wangeyaokoa tu maisha yao wenyewe kwa ajili ya haki yao. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Ataunyanganya utajiri wako pamoja na biashara yako. Atazibomoa kuta zako na kuziangusha nyumba zako nzuri; mawe, mbao na udongo ulivyotumia kwa kujenga nyumba hizo watavitupa katika bahari.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Kiro wa Persia, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, alipewa ufunuo. Ufunuo huo ulikuwa wa kweli, lakini ulikuwa mugumu sana. Hata hivyo alielewa ufunuo huo maana alifahamu maono vilevile.
“Mutamwona yeye anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ yule aliyetajwa na nabii Danieli, akisimamishwa katika hekalu. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake.)