Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 9:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Ee Yawe, utusikie; utusamehe ee Yawe. Ee Yawe, kwa ajili ya heshima yako utusikie na utende, wala usikawie, ee Mungu wangu, kwa ajili ya muji huu na watu hawa wanaoitwa kwa jina lako!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 9:19
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sikia maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watu wako Waisraeli wanapoomba wakielekea pahali hapa. Usikilize maombi kutokea kule mbinguni na ukisha kusikia, usamehe.


basi, ninakusihi usikilize ukiwa kule mbinguni maombi yao na malalamiko yao na uwapatie haki zao tena uwasamehe watu wako ambao wametenda zambi mbele yako.


Kila mumoja anajulikana kwa jina langu; niliwaumba wote na kuwafanya kwa ajili ya utukufu wangu.”


Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.


Namna gani unakuwa kama mutu aliyechanganyikiwa, kama shujaa asiyeweza kusaidia mutu? Ingawa hivyo wewe ee Yawe unakaa katikati yetu; nasi tunajulikana kwa jina lako, usituache.


Ikiwa ninaanza kuleta hasara katika muji unaojulikana kwa jina langu, basi ninyi munazani kwamba munaweza kuepuka azabu? Hamutaachwa bila kuazibiwa, maana ninaleta mauaji juu ya wakaaji wote wa dunia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa ambao waliona jinsi nilivyowatoa Waisraeli katika inchi ya Misri.


Lakini nilizuiza mukono wangu kwa sababu ya heshima ya jina langu kusudi nisizarauliwe kati ya watu wa mataifa walioona nikiwatoa katika inchi ya Misri.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.


Basi, uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninachotaka kufanya si kwa faida yenu ninyi watu wa inchi ya Israeli, lakini ni kwa heshima ya jina langu takatifu mulilolikufuru kati ya mataifa mulikokwenda.


Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi: Sasa nitawahurumia Waisraeli wazao wa Yakobo, na kuwarudishia fanaka yao. Ninataka jina langu takatifu liheshimiwe siku zote.


Tega sikio, ee Mungu wangu; angalia uone taabu tunazokuwa nazo na jinsi huo muji unaoitwa kwa jina lako unavyotaabika. Tunakutolea maombi yetu si kwa sababu tumetenda haki, lakini kwa sababu wewe una huruma nyingi.


Niliwaona nzige hao wakikula na kumaliza kila jani katika inchi. Halafu nikasema: Ee Bwana wetu Yawe, ninakusihi utuhurumie! Wazao wa Yakobo wataweza kuishi namna gani? Wao ni wadogo sana!


Ninakusihi uwasamehe watu hawa zambi zao, kadiri ya wema wako mwingi kama vile ulivyowasamehe tangu watoke Misri mpaka sasa.


Ndivyo watakavyotamka jina langu juu ya Waisraeli, nami nitawabariki.


Hakika ninawaambia kwamba hataamuka kumupatia mikate kwa sababu yeye ni rafiki yake tu, lakini sababu ya kusihi sana kwa rafiki yake, ataamuka na kumupatia vyote anavyohitaji.


kusudi watu wote wengine wamugeukie Bwana, watu wa mataifa yote wapate kuwa watu wangu wa pekee.


Kwa hiyo sisi tuliotangulia kumutumainia Kristo, tumusifu Mungu kwa ajili ya utukufu wake!


Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.


Lakini sasa, kwa njia ya kanisa, watawala na wote wenye uwezo wanaokuwa katika eneo la mbingu wapate kutambua hekima ya Mungu inayokuwa ya namna nyingi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ