Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 8:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Maono ya hizo nyakati za magaribi na za asubui ambayo yameelezwa ni ya kweli. Lakini uyafiche, sababu ni siri, maana yatatokea kisha siku nyingi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 8:26
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wote watakusanywa kama wafungwa katika shimo; watafungwa katika kifungo pamoja kwa miaka mingi, na kisha muda huo atawaazibu.


Wewe mwanadamu, Waisraeli wanafikiri kwamba maono yako yanahusu siku za nyuma sana, na unabii wako unahusu nyakati za mbali sana!


Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Kiro wa Persia, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, alipewa ufunuo. Ufunuo huo ulikuwa wa kweli, lakini ulikuwa mugumu sana. Hata hivyo alielewa ufunuo huo maana alifahamu maono vilevile.


nami nimekuja kukusaidia upate kuyafahamu mambo yatakayowapata watu wako wakati unaokuja, maana maono uliyoona yanaelekea wakati unaokuja.


Sasa nitakuelezea ule ukweli wa mambo haya. Wafalme wengine watatu wataitawala inchi ya Persia. Hao watafuatwa na mufalme wa ine ambaye atakuwa tajiri kuliko wale waliomutangulia. Wakati atakapopata nguvu kwa ajili ya utajiri wake, ataanza kuushambulia ufalme wa Ugriki.


Lakini sasa, Danieli, weka kwa siri mambo hayo; funga kitabu na kutia muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho utakapofika. Wengi watakimbilia huko na huko, na maarifa yataongezeka.


Akanijibu: Danieli, ujiendee, maana maneno haya ni siri na yamefungwa kwa kutiwa muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho.


Na ngurumo zile saba zilipokwisha kusikilika, nikajitayarisha kwa kuandika. Lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni, ikiniambia hivi: “Uchunge kwa siri maneno yaliyosemwa na zile ngurumo saba.”


Kisha akaniambia: “Usichunge kwa siri maneno haya ya unabii wa kitabu hiki, kwa sababu wakati wa kutimia kwa mambo haya unakaribia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ