Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 8:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Wakati falme hizo zitakapofikia kwa mwisho wao na uovu wao kufikia kilele chake, kutatokea mufalme mumoja mutesaji na mwerevu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 8:23
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wazao wako watarudi hapa katika kizazi cha ine, kwa sababu uovu wa Waamori haujakamilika bado.”


Wataweza kuelewa mezali na maana iliyofichwa, watayaelewa maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.


Utawashambulia Waisraeli, kama vile wingu linalotanda juu ya inchi. Wakati huo nitakutuma uishambulie inchi yangu, kusudi mataifa yajue kwamba nimekutumia wewe Gogi kusudi nionyeshe utakatifu wangu mbele yao.


Kisha siku nyingi utaitwa kuishambulia inchi ambayo watu wengi waliletwa kutoka mataifa mengi na sasa wanaishi bila vitisho vya vita. Utaishambulia milima ya Israeli ambayo hapo zamani ilikuwa jangwa na matongo kwa muda murefu, lakini sasa watu wote huko wanaishi kwa usalama.


nami nimekuja kukusaidia upate kuyafahamu mambo yatakayowapata watu wako wakati unaokuja, maana maono uliyoona yanaelekea wakati unaokuja.


Mufalme atakayefuata atakuwa wa kuzarauliwa ambaye asiyeweza kupewa heshima ya kifalme, naye atakuja wakati watu wasiouzania na kunyanganya ufalme kwa werevu.


Na kwa wakati wasiouwazia ataingia katika sehemu za jimbo zenye utajiri mwingi na kufanya mambo ambayo hayakufanyika hata na mumoja wa babu zake waliomutangulia. Kisha, atawagawanyia wafuasi wake mali na vitu alivyonyanganya katika vita. Atafanya mipango ya kuishambulia miji yenye kuta, lakini kwa muda tu.


Kutokana na maneno ya kujivuna yaliyokuwa yanasemwa na ile pembe, nikaendelea kuangalia. Nikaona yule nyama wa ine akiuawa, mwili wake ukaharibiwa na kutolewa uchomwe kwa moto.


Vilevile nilitaka nielezwe juu ya zile pembe kumi alizokuwa nazo juu ya kichwa chake, na ile pembe moja iliyoota na pembe zingine tatu zilizoanguka mbele yake, ndiyo ile pembe iliyokuwa na macho na kinywa ambacho kilisema maneno ya kujivuna, na ambayo ilionekana kuwa kubwa kuliko pembe zingine.


Huyo atasema maneno ya kujivuna mbele ya Mungu Mukubwa na kuwatesa watakatifu wake. Atajaribu kubadilisha sikukuu na sheria zao, na watakatifu watatiwa katika mikono yake kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


Nilipokuwa ninaziangalia hizo pembe, niliona pembe ingine ndogo ikiota katikati ya zile kumi, nayo ikaongoa pembe tatu kati ya hizo za kwanza. Pembe ile ilikuwa na macho ya kimutu na kinywa kilichosema maneno ya kujivuna.


Ile pembe iliyovunjika na pahali pake kukaota pembe ine, ina maana kwamba ufalme huo mumoja utagawanyika kuwa falme ine, lakini falme hizo hazitakuwa na nguvu kama ule ufalme wa kwanza.


Atakuwa mwenye mamlaka makubwa, atasababisha uharibifu mubaya sana, na atafanikiwa katika kila atakalotenda. Atawaangamiza watu wenye uwezo na watakatifu wa Mungu.


Kwa werevu wake, atafanikiwa katika mipango yake ya udanganyifu, naye atajitukuza. Atawaangamiza watu wengi sana, na atataka kupigana na Mukubwa wa wakubwa, lakini ataangamizwa pasipo kutumia nguvu za kimutu.


Mashua zitafika kutoka Kitimu, wataishambulia Asuria na Eberi, lakini nao vilevile wataangamia milele.


Basi mutimize hayo mambo babu zenu waliyoyaanza!


Watu wa taifa hilo watakuwa na nyuso kali. Hawatajali wazee wala kuwahurumia vijana.


Wanajikaza kutuzuiza tusitangaze Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kusudi wasiokoke. Hivi wanafikilia kwenye hatua ya mwisho ya zambi walizotenda siku zote. Lakini kwa mwisho kasirani ya Mungu imewaangukia.


Roho Mutakatifu anasema wazi kwamba katika nyakati za mwisho, watu wengine watapotoka katika imani yao na kufuata roho za udanganyifu na mafundisho ya pepo.


Yule nyama akakamatwa pamoja na yule nabii wa uongo aliyeonyesha vitambulisho mbele yake. (Ni kwa njia ya vitambulisho vile aliwadanganya wale waliopigwa chapa ya yule nyama na wale walioabudu sanamu yake.) Nyama yule pamoja na nabii wa uongo wakatupwa wangali wazima katika ziwa la moto munamowaka mawe ya kiberiti.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ