Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 7:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kisha, katika maono hayo yangu ya usiku, nikaona nyama wa ine wa ajabu na wa kutisha, mwenye nguvu sana. Huyu alikuwa na meno makubwa ya chuma ambayo aliyatumia kwa kula na kuvunjavunja, na mabaki aliyakanyagakanyaga. Alikuwa tofauti na wale nyama wengine watatu, maana alikuwa na pembe kumi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 7:7
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Niliwatwanga, wakakuwa kama mavumbi, nikawaponda na kuwakanyaga kama matope katika barabara.


Shingo yake ina nguvu ajabu, nyama yule anapotokea watu wanapatwa na hofu.


Basi, nikiwa katika maono Yawe akanipeleka mpaka katika inchi ya Israeli, akaniweka juu ya mulima murefu sana, na upande wa kusini kulikuwa majengo yaliyoonekana kama muji.


Halafu Danieli akafunuliwa fumbo hilo usiku katika maono. Naye Danieli akamushukuru Mungu wa mbinguni,


Wakati wa maono haya usiku, niliona kiumbe kinachofanana na mwanadamu. Akakuja katika mawingu na kumwendea yule Muzee wa zamani sana. Akakaribishwa mbele yake.


Mimi Danieli niliona maono usiku. Ilikuwa hivi: Upepo ulivuma juu ya bahari kubwa toka pande zote ine za mbinguni.


Pembe dogo ile ilikomaa sana kufikia viumbe vya mbinguni; ikaangusha chini sehemu ya nyota na kuzikanyagakanyaga.


Ile pembe iliyovunjika na pahali pake kukaota pembe ine, ina maana kwamba ufalme huo mumoja utagawanyika kuwa falme ine, lakini falme hizo hazitakuwa na nguvu kama ule ufalme wa kwanza.


Kisha kukaonekana kitambulisho kingine mbinguni. Kulikuwa nyoka mukubwa mwekundu mwenye vichwa saba na pembe kumi. Juu ya kila kichwa kulikuwa taji saba.


Kisha nikaona nyama mumoja wa ajabu akitokea ndani ya bahari. Alikuwa na vichwa saba na pembe kumi. Na juu ya kila pembe lake kulikuwa taji, na juu ya vichwa vile kulikuwa kumeandikwa jina la kumutukana Mungu.


“Zile pembe kumi ulizoona ni wafalme kumi, ambao hawajaanza bado kutawala, lakini watapewa mamlaka ya kutawala kama wafalme kwa muda wa saa moja pamoja na yule nyama.


Halafu yule malaika akaniuliza: “Kwa nini unashangaa? Nitakuambia maana ya fumbo la mwanamuke yule na ya yule nyama anayemubeba, na anayekuwa na vichwa saba na pembe kumi.


Yule nyama uliyemwona alikuwa yuko zamani, lakini sasa hayuko tena. Naye ni tayari kupanda toka katika shimo la kuzimu na kwenda kuangamizwa kabisa. Nao wakaaji wa dunia ambao majina yao hayakupata kuandikwa katika kitabu cha uzima tangia kuumbwa kwa dunia, watashangaa wakati watakapomwona yule nyama, kwa sababu alikuwa yuko zamani lakini hayuko sasa, naye atatokea tena!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ