Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 7:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Nilipokuwa nikiangalia, pembe hio ilipigana vita na watakatifu, nayo ikawashinda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 7:21
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waaskari wake watalichafua hekalu na kuta zake, watakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto za kila siku na kusimamisha kule katika hekalu chukizo linaloleta uharibifu.


Yule mutu aliyesimama upande wa juu wa muto, aliyevaa nguo za kitani, akainua mikono yake yote miwili kuelekea mbinguni. Kisha nikamusikia akiapa kwa jina la yule anayeishi milele: Itakuwa muda wa nyakati tatu na nusu. Wakati mateso ya watu watakatifu yatakapokomeshwa, mambo haya yote yatakuwa yametimia.


Vilevile nilitaka nielezwe juu ya zile pembe kumi alizokuwa nazo juu ya kichwa chake, na ile pembe moja iliyoota na pembe zingine tatu zilizoanguka mbele yake, ndiyo ile pembe iliyokuwa na macho na kinywa ambacho kilisema maneno ya kujivuna, na ambayo ilionekana kuwa kubwa kuliko pembe zingine.


Viumbe vya mbinguni vikatiwa chini ya mamlaka yake pamoja na sadaka za kuteketezwa kwa moto za kila siku, kwa ajili ya upotovu. Nao ukweli ukatupwa chini. Pembe dogo ile ikaiangusha chini ibada ya kweli. Ilifanikiwa katika kila jambo iliyofanya.


Atakuwa mwenye mamlaka makubwa, atasababisha uharibifu mubaya sana, na atafanikiwa katika kila atakalotenda. Atawaangamiza watu wenye uwezo na watakatifu wa Mungu.


Na tokea ndani ya moja ya pembe hizo ine, kuliota pembe ingine dogo, ikakomaa sana kuelekea upande wa kusini-mashariki, na kuelekea inchi ile nzuri sana.


Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”


Nikaona kwamba yule mwanamuke amelewa kwa damu ya watu wa Mungu na ya watu waliouawa kwa sababu ya ushuhuda wao kwa ajili ya Yesu. Wakati nilipomwona nikashangaa sana.


Nikaona yule nyama wa ajabu pamoja na wafalme wa dunia na makundi yao ya waaskari wamekusanyika pamoja kupigana vita na yule anayepanda juu ya farasi na kundi la waaskari wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ