Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 6:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Basi, hao wakubwa na maliwali wote pamoja, wakamwendea mufalme na kumwambia: Uishi milele ee mufalme Dario!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 6:7
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

anajificha katika maficho yake kama simba. Anavizia apate kuwakamata wamasikini; anawanasa kwa mutego wake na kuwachukua.


Wafalme wa dunia wanajitayarisha, watawala wanashauriana pamoja kumwasi Yawe na muchaguliwa wake.


Uniokoe na hao wanaotenda maovu, Uniponyeshe kutoka hao wauaji!


Ingawa sina kosa, wanakimbia, ee Yawe, kujiweka tayari. Uinuke, ee Yawe, uwaangalie na kunisaidia!


Mpaka wakati gani mutanishambulia mimi? Mpaka wakati gani ninyi wote mutanipiga, mimi ninayekuwa kama kiambaza kilichoinama, kama ukuta unaoanza kubomoka?


Wanasema: “Mukuje tuangamize taifa lao, hata jina la Israeli lisikumbukwe tena.”


Wewe hauwezi kushirikiana na waamuzi wapotovu, wanaotunga masharti za kutetea maovu.


Wale Wakaldea wakamwambia mufalme katika luga ya Kiaramu: Uishi milele, ee mufalme! Utuelezee ndoto yako nasi watumishi wako tutakufasiria maana yake.


Na kwamba mutu yeyote asiyeinama chini na kuiabudu sanamu hiyo, atupwe ndani ya furu la moto mukali.


Kisha mufalme akaamuru maliwali, wasimamizi, watawala, washauri, walinzi wa mali, waamuzi, wana sheria na wakubwa wote wa majimbo wahuzurie sikukuu ya kuzindua sanamu aliyosimamisha.


Maliwali, wasimamizi, wakubwa wa majimbo na washauri wa mufalme, wote wakakusanyika pamoja, wakaona kwamba ule moto haukuweza kuwaunguza hao watatu. Nywele zao hazikuungua, nguo zao hazikuungua wala hawakuwa na harufu yoyote ya moto.


Na yeyote ambaye hatainama chini na kuiabudu, atatupwa mara moja katika furu la moto mukali.


Wale watu kwa pamoja wakamwendea mufalme Dario na kumwambia: Ee mufalme, ujue kwamba hakuna sheria wala amri yoyote ya Wamedi na Wapersi inayoweza kubadilishwa kisha kuwekwa na mufalme.


Danieli akamujibu mufalme: Uishi milele, ee mufalme!


Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!


Basi lile pango la simba limekuwa namna gani, lile lililokuwa maficho ya simba wakali? Ile nafasi ya simba imekuwa namna gani, nafasi ya wana-simba ambayo hakuna aliyeweza kuwashitua?


Wafarisayo wakaondoka pale na kwenda kufanya shauri la kumwua Yesu.


nao wakafanya shauri la kumukamata Yesu kwa werevu na kumwua.


Asubui mapema, mara moja wakubwa wa makuhani wakafanya shauri pamoja na wasimamizi wa watu, walimu wa Sheria na wakubwa wote wa baraza. Wakamufunga Yesu, wakamupeleka na kwenda kumutoa kwa Pilato.


Basi wakubwa wa makuhani wakakata shauri la kumwua Lazaro vilevile,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ