Mpaka wakati gani mutanishambulia mimi? Mpaka wakati gani ninyi wote mutanipiga, mimi ninayekuwa kama kiambaza kilichoinama, kama ukuta unaoanza kubomoka?
Kisha mufalme akaamuru maliwali, wasimamizi, watawala, washauri, walinzi wa mali, waamuzi, wana sheria na wakubwa wote wa majimbo wahuzurie sikukuu ya kuzindua sanamu aliyosimamisha.
Maliwali, wasimamizi, wakubwa wa majimbo na washauri wa mufalme, wote wakakusanyika pamoja, wakaona kwamba ule moto haukuweza kuwaunguza hao watatu. Nywele zao hazikuungua, nguo zao hazikuungua wala hawakuwa na harufu yoyote ya moto.
Wale watu kwa pamoja wakamwendea mufalme Dario na kumwambia: Ee mufalme, ujue kwamba hakuna sheria wala amri yoyote ya Wamedi na Wapersi inayoweza kubadilishwa kisha kuwekwa na mufalme.
Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!
Basi lile pango la simba limekuwa namna gani, lile lililokuwa maficho ya simba wakali? Ile nafasi ya simba imekuwa namna gani, nafasi ya wana-simba ambayo hakuna aliyeweza kuwashitua?
Asubui mapema, mara moja wakubwa wa makuhani wakafanya shauri pamoja na wasimamizi wa watu, walimu wa Sheria na wakubwa wote wa baraza. Wakamufunga Yesu, wakamupeleka na kwenda kumutoa kwa Pilato.