Danieli 6:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
6 Halafu wakapatana hivi: Hatutapata kisingizio chochote cha kumushitaki Danieli isipokuwa kama kisingizio hicho kitakuwa kinaelekea Sheria ya Mungu wake.
Nikamujibu: “Ee mufalme, uishi milele! Kwa nini nisikuwe mwenye huzuni wakati Yerusalema ambamo makaburi ya babu zangu uko tupu na milango yake imeteketezwa kwa moto?”
Kutokana na kelele za mufalme na wakubwa wake, mama ya mufalme aliingia ndani ya chumba cha karamu, akasema: Uishi milele, ee mufalme! Si lazima mawazo yako yakufazaishe na rangi yako kubadilika.
Danieli alipojua kwamba ile sheria imetiwa sahihi, alirudi kwa nyumba yake kwenye gorofi katika chumba chake kilichokuwa na madirisha yaliyofunguka kuelekea Yerusalema. Humo, Danieli, kama ilivyokuwa kawaida yake, alipiga magoti mara tatu kila siku kwa kuomba na kumushukuru Mungu wake.
Alipofika karibu akamwita Danieli kwa sauti ya huzuni: Danieli, mutumishi wa Mungu Mwenye Uzima, Mungu wako unayemutumikia siku zote ameweza kukuokoa na simba hawa?
Walipomwita Paulo, Tertulo akaanza kumushitaki, akisema: “Muheshimiwa Feliki, kwa njia yako tumepata amani ya kweli. Na kwa uongozi wako umeleta mabadiliko mengi mazuri kwa ajili ya taifa hili.