Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 6:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Danieli akaonekana kuwa bora kuliko wale wasimamizi wengine na wakubwa wote kwa maana alikuwa na roho njema. Hivyo mufalme akakusudia kumupa uongozi wa ufalme wote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 6:4
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo mufalme akawauliza watumishi wake: “Huyu mutu ana roho wa Mungu! Tunaweza kumupata mutu mwingine kama huyu?”


Walipoona wamepelekwa kwenye nyumba ya Yosefu, wakashikwa na hofu, wakasema wao kwa wao: “Tumeletwa huku kwa sababu ya ile feza tuliyorudishiwa katika mifuko yetu tulipokuja safari ya kwanza kusudi apate kisingizio cha kutushambulia kwa rafla na kutunyanganya punda wetu na kutufanya watumwa wake.”


Mwovu ni chukizo kwa mwenye haki, naye mwenye haki ni chukizo kwa mwovu.


Tena nilitambua kwamba mutu anatoa jasho na kutumia ujuzi wake juu ya wivu tu kwa mwenzake. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.


Lakini wewe, ee Yawe, unajua mashauri yao ya kuniua. Usiwasamehe uovu wao, wala kufuta zambi zao. Waanguke chini mbele yako; uwapige wakati wa hasira yako.


Ninasikia watu wengi wakinisingizia uongo, nao wananipanga jina la Kitisho Kila Pahali! Wengine wanasema: Tumushitaki, Tumushitaki! Rafiki zangu wapenzi wote wanangojea kwa hamu nianguke! Wanasema: Labda atadanganyika, tupate kumunasa na kumulipiza kisasi.


Mushugulike na kuleta ustawi katika muji ule ambamo nimewahamishia. Muuombee muji huo kwa Yawe, maana ukistawi ninyi vilevile mutastawi.


Wakati huo, watu wamoja kati ya Wakaldea wakajitokeza na kuwashitaki Wayuda. Walimwambia mufalme Nebukadneza:


kwa sababu ana roho njema, maarifa, ujuzi wa kufasiria ndoto, kufumbua mafumbo na kutatua matatizo. Jina la mutu huyo ni Danieli ambaye baba yako alimwita Beltesaza. Basi wamwite, naye atakuelezea maana ya maandiko haya.


Danieli akamujibu mufalme: Uishi milele, ee mufalme!


nao wakafanya shauri la kumukamata Yesu kwa werevu na kumwua.


Alisema vile kwa maana alijua kwamba walimutoa Yesu kwake kwa sababu walimwonea wivu tu.


Basi wakaanza kumuvizia Yesu, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa kama watu wazuri kusudi wamunase katika masemi. Na kwa njia ile waweze kumutoa katika mikono ya watawala wa inchi.


Basi watu wale hawakuweza kumunasa katika neno lolote mbele ya watu, lakini wakashangaa na jibu lake, nao wakanyamaza.


Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walitafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliogopa watu.


Pilato akatoka tena inje na kuwaambia Wayuda: “Angalia, nitawaletea naye hapa inje kusudi mupate kujua kwamba mimi sioni hata sababu moja ya kumuhukumu.”


Nitaendelea kufanya sawasawa ninavyofanya kwa sasa, kusudi niwafungie njia zote wale wanaotafuta kujivuna kwamba wanatumika sawa sisi.


kusudi mupate kuwa bila kosa na kuwa na maisha safi. Hivi mutakuwa watoto wakamilifu wa Mungu wasiokuwa na kilema kati ya watu waovu na wapotovu wa dunia hii. Munapaswa kuangaza kati ya watu hawa kama vile nyota zinavyoangaza katika mbingu,


Kwa sababu hiyo, ninataka wajane wanaokuwa wangali vijana waolewe, wazae watoto na kutunza nyumba zao, kusudi waadui wasipate nafasi ya kutuchongea.


Ufundishe maneno ya kweli watu wasiyoweza kubishia, hata wale wanaokupinga wapate haya kwa kukosewa na neno baya la kusema juu yetu.


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


mukiwa na zamiri safi, hata wale wanaowasingizia na kuwatukana juu ya mwenendo wenu muzuri katika ushirika wenu na Kristo, wapate haya.


Wazazi wake hawakujua kwamba ule ulikuwa mupango wa Yawe ambaye alikuwa anatafuta njia ya kushambulia Wafilistini. Wakati ule, Wafilistini walikuwa wakiwatawala Waisraeli.


Watu wakamujibu: “Haujatudanganya hata kidogo, haujatugandamiza, wala haujakamata kitu chochote kwa mutu.”


Daudi alifanikiwa katika kila kitu alichofanya, maana Yawe alikuwa pamoja naye.


Ahimeleki akamujibu: “Kati ya watumishi wako, Daudi ndiye mukubwa wa kuaminika kuliko wote. Yeye ni mukwe wako wewe mufalme mwenyewe, mukubwa wa waaskari wako walinzi na anaheshimiwa kuliko wote katika nyumba yako.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ