Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 6:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Kwa hiyo mufalme akafurahi sana; akaamuru kwamba wamwondoe Danieli toka ndani ya pango. Basi wakamwondoa, naye hakuonekana na alama hata kidogo ya kidonda, kwa sababu alimutegemea Mungu wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 6:24
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini hakuwaua watoto wa wauaji kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa, Yawe alipotoa amri akisema: “Wazazi hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya wazazi wao; lakini kila mutu atauawa kwa ajili ya zambi zake mwenyewe.”


Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.


wana kumi wa Hamani mwana wa Hamedata, adui ya Wayuda. Hata hivyo, hawakunyanganya mali zao.


Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.


Watu wenye kiburi wananishambulia, watu wakali wanawinda maisha yangu, watu ambao hawamujali Mungu.


Mutu wa haki anaokolewa katika shida, na mwovu anaingia mule kwa pahali pake.


Mushuhuda mwongo hatakosa kuazibiwa; anayesema uongo ataangamia.


Usiku kucha nililia kwa kuomba musaada; kama simba, anavunjavunja mifupa yangu; muchana na usiku ananikomesha.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninyi hamukunitii juu ya kuwapatia wandugu zenu Waisraeli uhuru. Basi, nami vilevile nitawapatia ninyi uhuru: uhuru wa kuuawa kwa upanga katika vita, kuuawa kwa ugonjwa mukali na kwa njaa. Nitawafanya ninyi kuwa kitambulisho cha kuogopesha kwa falme zote katika dunia.


Kwa vile amri ya mufalme ilikuwa kali, ule moto ulikuwa umewashwa na kuwa mukali sana, hata ndimi za moto zikawateketeza wale watu waliowapeleka Sadiraki, Mesaki na Abedenego.


“Wazazi wasiuawe kwa makosa ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya makosa ya wazazi wao. Kila mutu atauawa kwa makosa yake mwenyewe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ