Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 6:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mufalme Dario aliamua kuweka wakubwa mia moja na makumi mbili kwa kusimamia mambo ya ufalme.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 6:2
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tena, muangalie sana musichelewe kufanya hivyo, kusudi nisipate hasara.


Maana, mimi na watu wangu tumeuzishwa kusudi tuuawe, tuangamizwe na kuteketezwa kabisa. Kama tungeuzishwa tu kuwa watumwa na wajakazi, ningekaa kimya wala nisingekusumbua. Ingawa tutateswa hakuna adui atakayeweza kulipa hasara hii kwa mufalme.”


Kutuma ujumbe kwa mukono wa mupumbafu ni kama kujikata miguu au kujitafutia mateso.


Lakini, nimesikia kwamba wewe unaweza kueleza vitendawili na kutambua mafumbo. Basi, kama ukiweza kusoma maandiko haya na kunielezea maana yake, utavalishwa nguo nzuri ya rangi nyekundu na kuvalishwa mukufu wa zahabu katika shingo lako. Utapewa nafasi ya tatu katika ufalme huu.


Pale pale, mufalme Belsasari akaamuru kwamba Danieli avalishwe nguo nzuri nyekundu na mukufu wa zahabu katika shingo. Ikatangazwa kwamba Danieli atakamata sasa nafasi ya tatu katika ufalme.


Mufalme Belsasari akaamuru kwa sauti kwamba wachawi, Wakaldea wenye hekima na waaguzi waletwe. Walipoletwa, mufalme akawaambia wenye hekima hao wa Babeli: Yeyote atakayesoma maandiko haya na kunijulisha maana yake, atavalishwa nguo nzuri nyekundu za kifalme na mukufu wa zahabu katika shingo lake, na kupewa nafasi ya tatu katika ufalme.


Naye mufalme Dario, wa inchi ya Wamedi, akatwaa utawala akiwa na umri wa miaka makumi sita na miwili.


Ni kwa sababu hii Ufalme wa mbinguni unafanana na mufalme mumoja aliyetaka kufanya hesabu ya madeni watumishi wake waliyokuwa nayo.


Halafu bwana wake akamwita na kumwambia: ‘Ni habari gani ile waliyonielezea juu yako? Ninakuomba unifanyie hesabu yote ya mali yangu, kwa sababu hauwezi tena kuwa mulinzi wa mali yangu.’


Yanayohitajika kwa mwenye madaraka kama hayo, ni kuwa mwaminifu.


Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ