Danieli 6:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
17 Halafu mufalme Dario akatoa amri, naye Danieli akaletwa na kutupwa katika pango la simba. Mufalme akamwambia Danieli: Mungu wako ambaye unamutumikia siku zote akuokoe.
Alipokwisha kumukamata Petro, na kumutia katika kifungo, akamuweka chini ya ulinzi wa vikundi vine vya waaskari waliogomboana wane kwa wane. Naye alikusudia kumusambisha mbele ya watu nyuma ya sikukuu ya Pasaka.
Malaika yule akamutupa ndani ya shimo ndefu la kuzimu. Akalifunga na kutia kitambulisho cha muhuri juu yake kwamba lisifunguliwe kusudi nyoka yule asiyadanganye tena mataifa mpaka ile miaka elfu moja ipate kutimia. Kisha miaka hiyo, anapaswa kufunguliwa tena kwa muda mufupi.