Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 5:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 PERESI: ufalme wako umegawanywa kati ya Wamedi na Wapersi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 5:28
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Hivi ndivyo anavyosema Kiro mufalme wa Persia: ‘Yawe, Mungu wa mbingu, amenipatia falme zote za ulimwengu, na ameniagiza nimujengee nyumba katika Yerusalema, katika inchi ya Yuda. Basi sasa kila mutu kati yenu, ninyi wote munaokuwa watu wa Yawe, Mungu wake akuwe pamoja naye, na aende.’ ”


Ninawachochea Wamedi juu yao; watu ambao hawajali feza wala hawavutwi na zahabu.


Nimeonyeshwa maono ya kutisha: wadanganyifu wanadanganya na waangamizaji wanaangamiza. Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu! Mushambulie, enyi Wamedi! Mungu atakomesha mateso yote yaliyoletwa na Babeli.


Lakini hasara itakupata ambayo hautaweza kujiepusha nayo. Magumu yatakutokea ambayo hautaweza kuyapinga; maangamizi yatakufikia kwa rafla ambayo haujapata kuyaona hata kidogo.


Nitaleta juu ya inchi hiyo mambo yote niliyosema juu yake na yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki ambayo Yeremia alitabiri juu ya mataifa yote.


Mutayarishe mataifa kwa kupigana naye vita; muwatayarishe wafalme wa Medi, watawala na maliwali wao, mutayarishe inchi zote katika utawala wao.


Kichwa cha sanamu hiyo kilikuwa cha zahabu safi, kifua chake na mikono yake vilikuwa vya feza na tumbo lake na mapaja yake vilikuwa vya shaba.


Nyuma yako kutafuata ufalme mwingine, lakini ufalme huo utakuwa zaifu. Huu utafuatwa na ufalme wa tatu unaofananishwa na shaba; huo utaitawala dunia yote.


Yeye anakomboa na kuokoa, anafanya miujiza na maajabu mbinguni na katika dunia, maana amemwokoa Danieli toka nguvu za simba.


Sisi wakubwa uliotuweka, wasimamizi, maliwali, washauri na wakubwa wa majimbo, wote tumepatana kwamba inafaa, ee mufalme, utoe amri na kuhakikisha kwamba inafuatwa kikamilifu. Amuru kwamba kwa muda wa siku makumi tatu kusikuwe mutu yeyote atakayeruhusiwa kuomba kitu chochote kwa mungu yeyote au kwa mutu yeyote, isipokuwa kutoka kwako wewe, ewe mufalme. Mutu yeyote atakayevunja sheria hii atupwe katika pango la simba.


Yule kondoo dume uliyemwona mwenye pembe mbili, ni wafalme wa Media na Persia.


Katika mwaka Dario mufalme wa Wamedi mwana wa Ahasuero, alipoanza kutawala juu ya ufalme wa Wakaldea,


Kati yetu kuna watu wenye kutoka katika inchi hizi: Parti, Medi, Elamu, Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto, Jimbo la Azia,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ