Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 5:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kutokana na kunywa divai, mufalme Belsasari akatoa amri kwamba vile vyombo vya zahabu na feza ambavyo baba yake mufalme Nebukadneza alivyokamata kutoka hekalu la Yerusalema, viletwe kusudi avitumie kwa kunywea divai pamoja na wakubwa wake, wanawake wake na wahabara wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 5:2
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi akamwambia: “Usiogope. Mimi nitakutendea mema kwa ajili ya baba yako Yonatani. Nitakurudishia yale mashamba yote yaliyokuwa ya babu yako Saulo. Nawe, utakula kwenye meza yangu siku zote.”


Tena kama vile Yawe alivyosema, Nebukadneza alitwaa mali yote iliyokuwa ndani ya nyumba ya Yawe, na ndani ya nyumba ya kifalme. Akakatakata vyombo vyote vya zahabu ambavyo Solomono mufalme wa Israeli alitengeneza. Vyombo hivyo vilikuwa ndani ya hekalu la Yawe.


wakapeleka vyetezo na mabakuli. Mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme akapeleka mbali kila chombo cha zahabu na kila chombo cha feza.


Kisha, akamwoa Maka binti ya Abusaloma, naye akamuzalia Abiya, Atai, Siza na Selomiti.


Mufalme Asa alimwondoa hata mama yake Maka, cheo chake cha malkia, kwa sababu alitengeneza sanamu ya kuchukiza ya Ashera, mungu wa kike. Asa alikatakata sanamu hiyo, akaipondaponda na kuiteketeza kwa moto katika bonde la kijito Kidroni.


Mwaka ulipokwisha, mufalme Nebukadneza alituma wajumbe, wakamuchukua Yoyakini na kumupeleka mpaka Babeli, pamoja na vyombo vya bei kali vya nyumba ya Yawe. Akamweka ndugu yake Sedekia kuwa mufalme wa Yuda na Yerusalema.


Alitwaa vyombo vyote vya nyumba ya Mungu vikubwa na vidogo na hazina ya nyumba ya Yawe na ya mufalme na wakubwa wake. Alivipeleka vyote mpaka Babeli.


Vilevile akavirudisha vyombo vya zahabu na feza ambavyo mufalme Nebukadneza alikuwa amevipeleka kutoka katika hekalu kule Yerusalema na kuviweka katika hekalu la Babeli. Vyombo hivyo Kiro akaviondoa toka hekalu la Babeli na kuvipatia Sesebasari ambaye alikuwa amemuchagua akuwe mutawala wa Yuda; akamwamuru akisema:


Mataifa yote yatamutumikia yeye, pamoja na mwana wake na mujukuu wake mpaka wakati inchi yake itakapoanguka. Kisha mataifa mengi na wafalme wengi wakubwa watamufanya kuwa mutumwa wao.


Upanga ukuwe juu ya Wakaldea, juu ya wakaaji wa Babeli na wakubwa na wenye hekima wake! –Ni ujumbe wa Yawe.–


Yule mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme alipeleka vibakuli, vyetezo, mabeseni, vyungu, vinara vya taa, vijiko vikubwa na mabakuli ya sadaka za vinywaji, vyombo hivyo vikiwa vya zahabu au vya feza.


Bwana akamwacha Yoyakimu atiwe katika mikono ya mufalme Nebukadneza pamoja na sehemu ya vyombo vya nyumba ya Mungu. Basi mufalme Nebukadneza akakamata wafungwa na vyombo akavipeleka katika inchi ya Babeli, akaviweka katika hazina ya nyumba ya miungu yake.


Katika ufalme wako kuna mutu ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake. Wakati wa utawala wa baba yako, mutu huyu alionekana kuwa mwenye ujuzi, ufahamu na hekima kama ya miungu. Baba yako, mufalme Nebukadneza, alimufanya kuwa mukubwa wa waaguzi, wachawi, Wakaldea wenye hekima, na waganga,


Basi, Danieli akaletwa mbele ya mufalme, naye mufalme akamwuliza: Wewe ndiwe Danieli, mumoja wa wafungwa ambao baba yangu mufalme, aliowaleta kutoka inchi ya Yuda?


Ee mufalme, Mungu Mukubwa alimupa baba yako mufalme Nebukadneza ufalme, ukubwa, mamlaka na utukufu.


Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


Basi, vile vyombo vya zahabu na feza vilivyokamatwa katika hekalu kule Yerusalema vikaletwa. Mufalme, wakubwa wake, wanawake wake na wahabara wake wakavitumia kwa kunywea.


Usiku uleule, mufalme Belsasari wa Wakaldea, aliuawa.


Walikunywa na kusifu sanamu za miungu iliyotengenezwa na zahabu, feza, shaba, chuma, miti na mawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ