Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 5:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Basi, Danieli akaletwa mbele ya mufalme, naye mufalme akamwuliza: Wewe ndiwe Danieli, mumoja wa wafungwa ambao baba yangu mufalme, aliowaleta kutoka inchi ya Yuda?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 5:13
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wote waliorudi kutoka katika uhamisho wakakubali mupango huo, kwa hiyo kuhani Ezra akawachagua wanaume kati ya viongozi wa ukoo mbalimbali na kuyaandika majina yao. Kwa siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, watu hao wakaanza kazi yao ya uchunguzi wa shauri hilo.


Tangazo likatolewa kila pahali katika inchi ya Yuda na Yerusalema kwa wote waliotoka katika uhamisho kwamba wakusanyike Yerusalema.


Kisha waadui za watu wa Yuda na Benjamina waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka katika uhamisho wanalijenga upya hekalu la Yawe, Mungu wa Israeli,


Basi, watu wa Israeli, makuhani, Walawi na watu wengine waliokuwa wamerudi kutoka katika uhamisho wakaizindua nyumba ya Mungu kwa shangwe kubwa.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Yoyakimu wa Yuda, mufalme Nebukadneza wa Babeli alikwenda Yerusalema, akauzunguka muji.


Bwana akamwacha Yoyakimu atiwe katika mikono ya mufalme Nebukadneza pamoja na sehemu ya vyombo vya nyumba ya Mungu. Basi mufalme Nebukadneza akakamata wafungwa na vyombo akavipeleka katika inchi ya Babeli, akaviweka katika hazina ya nyumba ya miungu yake.


Danieli alidumu katika kazi ya nyumba ya mufalme mpaka mwaka wa kwanza wa utawala wa mufalme Kiro.


Kati ya vijana waliochaguliwa kulikuwa Danieli, Hanania, Misaeli na Azaria, wote wa kabila la Yuda.


Basi, Arioki akamupeleka Danieli mbele ya mufalme kwa haraka na kumwambia: Nimemupata mutu fulani kati ya wafungwa wa Yuda anayeweza kukufasiria maana ya ndoto yako, ee mufalme.


Kisha mufalme Nebukadneza akamupandishia Danieli heshima kubwa, akamupa zawadi nyingi kubwakubwa, na kumufanya kuwa mutawala wa jimbo lote la Babeli, na mukubwa wa wenye hekima wote wa Babeli.


Katika ufalme wako kuna mutu ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake. Wakati wa utawala wa baba yako, mutu huyu alionekana kuwa mwenye ujuzi, ufahamu na hekima kama ya miungu. Baba yako, mufalme Nebukadneza, alimufanya kuwa mukubwa wa waaguzi, wachawi, Wakaldea wenye hekima, na waganga,


Nimesikia kwamba roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, na kwamba una ujuzi, na akili, na hekima ya ajabu.


Ee mufalme, Mungu Mukubwa alimupa baba yako mufalme Nebukadneza ufalme, ukubwa, mamlaka na utukufu.


Kutokana na kunywa divai, mufalme Belsasari akatoa amri kwamba vile vyombo vya zahabu na feza ambavyo baba yake mufalme Nebukadneza alivyokamata kutoka hekalu la Yerusalema, viletwe kusudi avitumie kwa kunywea divai pamoja na wakubwa wake, wanawake wake na wahabara wake.


Basi, walikwenda kwa mufalme na kumushitaki Danieli kwa kutumia ile sheria, wakisema: Mufalme Dario, haukutia sahihi kwenye sheria kwamba kwa muda wa siku makumi tatu hakuna mutu yeyote atakayeruhusiwa kuomba kitu chochote, kwa mungu yeyote, au kwa mutu yeyote isipokuwa kutoka kwako wewe, ee mufalme, na kwamba yeyote atakayevunja sheria hii atatumbukizwa katika pango la simba? Mufalme akaitikia: Hivi ndivyo inavyokuwa kulingana na sheria ya Wamedi na Wapersi ambayo haiwezi kuvunjika.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Belsasari, mimi Danieli nikapata maono mengine zaidi ya maono yale ya kwanza.


Mimi Danieli, nikazimia na kuugua kwa muda. Nilipopona, nikaendelea na shuguli za mufalme. Lakini yale maono yalishangaza, nami sikuweza kuyaelewa.


Kisha mambo hayo, Yesu akatembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea katika Yudea, kwa sababu Wayuda walitaka kumwua.


wandugu za Yesu wakamwambia: “Ondoka hapa, uende Yudea kusudi wanafunzi wako waone matendo unayofanya.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ