Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 5:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Katika ufalme wako kuna mutu ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake. Wakati wa utawala wa baba yako, mutu huyu alionekana kuwa mwenye ujuzi, ufahamu na hekima kama ya miungu. Baba yako, mufalme Nebukadneza, alimufanya kuwa mukubwa wa waaguzi, wachawi, Wakaldea wenye hekima, na waganga,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 5:11
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo mufalme akawauliza watumishi wake: “Huyu mutu ana roho wa Mungu! Tunaweza kumupata mutu mwingine kama huyu?”


Nami mujakazi wako nilifikiri hivi: ‘Neno la bwana wangu mufalme litanipa amani ndani ya moyo, maana wewe bwana wangu mufalme ni kama malaika wa Mungu katika kupambanua mazuri na mabaya.’ Yawe, Mungu wako, akuwe pamoja nawe.”


Wewe unajiona mwenye hekima kuliko Danieli, unazani hakuna siri yoyote usiyoijua.


Kwa hekima na akili yako umejipatia utajiri, umejikusanyia zahabu na feza ukaziweka katika hazina zako.


Mufalme alitaka vijana wasiokuwa na kilema, wazuri kwa umbo, wenye ujuzi wa kila hekima, wenye akili na maarifa na wanaofaa kwa kutumika katika nyumba ya kifalme. Alitaka vilevile vijana wale wafundishwe kusoma na kuandika luga ya Wakaldea.


Jambo unalouliza, ee mufalme, ni gumu. Hakuna mutu anayeweza kukufunulia isipokuwa miungu peke yake ambayo haikai kati ya wanadamu.


Anafunua siri na mafumbo, anajua kinachokuwa katika giza, mwangaza unakaa kwake.


majani yake yakiwa mazuri, na matunda yake mengi ya kukulisha viumbe vyote, nyama wa pori wakipata kivuli chini yake, na ndege wakikaa katika matawi yake,


Kisha, Danieli akafika, anayeitwa vilevile Beltesaza, jina la mungu wangu, ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake, nami nikamwelezea ndoto yangu, nikasema:


Ee Beltesaza, unayekuwa mukubwa wa waganga, ninafahamu kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, na kwamba hakuna fumbo linalokuwa gumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu; uniambie maana yake.


Nimesikia kwamba roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, na kwamba una ujuzi, na akili, na hekima ya ajabu.


Mufalme Belsasari akaamuru kwa sauti kwamba wachawi, Wakaldea wenye hekima na waaguzi waletwe. Walipoletwa, mufalme akawaambia wenye hekima hao wa Babeli: Yeyote atakayesoma maandiko haya na kunijulisha maana yake, atavalishwa nguo nzuri nyekundu za kifalme na mukufu wa zahabu katika shingo lake, na kupewa nafasi ya tatu katika ufalme.


Nao watu wakalalamika wakisema: “Hii ni sauti ya Mungu, wala si ya mutu.”


Wakati makundi ya watu walipoona jambo lile Paulo alilofanya, wakasema kwa sauti katika luga yao ya kilikaonia: “Miungu imetushukia ikiwa na sura ya kimutu!”


Siku moja tulipokuwa tukienda kule kwenye nafasi ya kufanyia maombi, tukakutana na mujakazi mumoja. Yule mwanamuke alikuwa na pepo wa kuaguza ndani yake. Na kwa njia ya uaguzi ule aliwatajirisha wabwana wake.


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ