Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Muti uliendelea kukomaa, ukakuwa imara na kilele chake kikafika mbinguni. Uliweza kuonekana kutoka kila pahali katika dunia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 4:8
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo mufalme akawauliza watumishi wake: “Huyu mutu ana roho wa Mungu! Tunaweza kumupata mutu mwingine kama huyu?”


Ule mungu Bali ameanguka; mungu Nebo anainama. Sanamu zao zinabebwa juu ya nyama, juu ya nyama wanaobeba mizigo! Vitu ninyi mulivyokuwa mukiviinua juu, vinakuwa sasa mizigo, vinakuwa mizigo mizito juu ya nyama wenye kuchoka.


Halafu walikumbuka siku za zamani, wakati wa Musa, mutumishi wa Yawe. Wakauliza: Yuko wapi sasa Yawe, aliyewaokoa wachungaji wa kundi lake katika bahari? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mutakatifu kati yao,


Mutangaze kati ya mataifa, munyanyue bendera na kutangaza, musifiche jambo lolote. Museme: Babeli umetekwa, mungu Beli amepatishwa haya. Merodaki amefazaishwa; sanamu zake zimefezeheshwa, miungu yake imefazaishwa.


Kweli, nitalipanda juu ya mulima murefu wa inchi ya Waisraeli kusudi lichanue na kuzaa matunda. Litakuwa mwerezi muzuri, na ndege wa aina zote watakaa chini yake vilevile watajenga chicha zao katika matawi yake.


Yule mukubwa wa watumishi akawapa majina mengine; akamwita Danieli kwa jina la Beltesaza, Hanania kwa jina la Sadiraki, Misaeli kwa jina la Mesaki na Azaria kwa jina la Abedenego.


Jambo unalouliza, ee mufalme, ni gumu. Hakuna mutu anayeweza kukufunulia isipokuwa miungu peke yake ambayo haikai kati ya wanadamu.


Mufalme akamwuliza Danieli, ambaye vilevile aliitwa Beltesaza: Unaweza kunijulisha ndoto niliyoota na maana yake?


Mufalme Nebukadneza akawauliza: Ni kweli kwamba wewe Sadiraki, wewe Mesaki na wewe Abedenego, hamwitumikii miungu yangu wala kuiabudu ile sanamu ya zahabu niliyoisimamisha?


majani yake yakiwa mazuri, na matunda yake mengi ya kukulisha viumbe vyote, nyama wa pori wakipata kivuli chini yake, na ndege wakikaa katika matawi yake,


Majani yake yalikuwa mazuri. Ulikuwa umejaa matunda mengi yaliyotoshelea kwa kulisha dunia nzima. Nyama wote wa pori walipata kivuli chini yake, na ndege wa anga walikaa katika matawi yake. Viumbe vyote vilipata chakula kutoka muti huo.


Nimesikia kwamba roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, na kwamba una ujuzi, na akili, na hekima ya ajabu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ