Moabu amestarehe tangu ujana wake, ametulia kama divai katika mutungi. Hajamimiliwa toka chombo kimoja katika chombo kingine, hajapata kupelekwa katika uhamisho. Kwa hiyo angali na onjo yake, harufu yake nzuri haijabadilika hata kidogo.
Ulikuwa na kiburi kwa sababu ya uzuri wako. Uliharibu hekima yako kwa sababu ya utukufu wako. Nilikutupa chini kwenye udongo, nikakufanya kuwa kitisho kwa wafalme.
Umwambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana na wewe mufalme wa Misri, wewe mamba unayelala ndani ya muto Nili! Wewe unafikiri kwamba muto Nili ni wako, kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!
Wakati huo nitauchunguza Yerusalema kwa taa, nitawaazibu wanaoishi wakitulia kama machicha ya divai, wote ambao wanasema kati yao: Yawe hatafanya kitu: chema au kibaya.