Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 4:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 4:34
57 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Matendo ya Mungu ni makamilifu. Ahadi ya Yawe ni ya kuaminika. Yeye ni ngao kwa wote wanaomukimbilia.


Halafu Daudi akamutukuza Yawe mbele ya mukutano wote, akisema: “Utukuzwe milele na milele, ee Yawe, Mungu wa baba yetu Israeli.


Sasa, ee Mungu wetu, tunakushukuru na kusifu jina lako tukufu.


akisema: Nilikuja uchi katika dunia, nitaondoka uchi katika dunia. Yawe amenipa, Yawe ametwaa. Jina la Yawe litukuzwe.


Yawe ni mufalme milele na milele! Mataifa yatatoweka katika inchi yake.


Mungu amenipunguzia nguvu ningali kijana; amefupisha maisha yangu.


Mumushukuru Yawe kwa wema wake na maajabu yake kwa wanadamu.


Wamutolee sadaka za shukrani; waeleze matendo yake kwa nyimbo za shangwe.


Mumushukuru Yawe kwa wema wake na maajabu yake kwa wanadamu.


Mumushukuru Yawe kwa wema wake na maajabu yake kwa wanadamu.


Matendo yake ni ya haki na ya kuaminika; kanuni zake zote ni za kutegemewa siku zote.


Wimbo wa safari za kidini. Ninainua macho kwenye milima. Musaada wangu unatoka wapi?


Wimbo wa safari za kidini. Ninainua macho kwako, ee Yawe, wewe unayeikaa huko juu mbinguni!


Ufalme wako ni ufalme wa milele; mamlaka yako yanadumu vizazi vyote. Yawe ni mwaminifu katika ahadi zake zote, ni mwema katika matendo yake yote.


Yawe anatawala milele. Mungu wako, ee Sayuni, ni mufalme kwa vizazi vyote! Haleluia!


Shukrani ikuwe ndiyo sadaka yako kwa Mungu. Umutimizie Mungu Mukubwa ahadi zako.


Anatawala milele kwa nguvu yake kubwa; macho yake yanachungulia mataifa yote. Mwasi yeyote asisubutu kumupinga.


Uharibifu wake utamurudilia yeye mwenyewe; ukali wake utamwangukia yeye mwenyewe.


Nitakushukuru wewe Mungu kwa moyo wangu wote; nitayaeleza matendo yako yote ya ajabu.


Yawe anasema hivi: Nitauazibu ulimwengu kwa uovu wake, waovu kwa sababu ya makosa yao. Nitakikomesha kiburi cha wenye majivuno, na kuporomosha mazarau ya watu wakali.


Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa, watu wenye majivuno watashushwa chini, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


na wale wa upande wa mashariki wanamusifu. Watu wa mbali wanalisifu jina la Yawe, Mungu wa Israeli.


Lakini Yawe ni Mungu wa kweli, Mungu Mwenye Uzima, mufalme wa milele. Akikasirika, dunia inatetemeka, mataifa hayawezi kuvumilia hasira yake.


Maovu na mema yanatokea tu kwa amri ya Mungu Mukubwa.


Yule mutu aliyesimama upande wa juu wa muto, aliyevaa nguo za kitani, akainua mikono yake yote miwili kuelekea mbinguni. Kisha nikamusikia akiapa kwa jina la yule anayeishi milele: Itakuwa muda wa nyakati tatu na nusu. Wakati mateso ya watu watakatifu yatakapokomeshwa, mambo haya yote yatakuwa yametimia.


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Lakini nikaota ndoto iliyonitisha; nikiwa nimelala katika kitanda, mawazo na maono yaliniogopesha.


Nyuma ya miezi kumi na miwili, mufalme Nebukadneza alikuwa anatembea juu ya dari ya nyumba ya kifalme katika muji wa Babeli.


Hivyo, nikaamuru wenye hekima wote wa Babeli waletwe mbele yangu kusudi wanielezee maana ya ndoto hiyo.


Wakaaji wote wa dunia si kitu; anafanya anavyotaka na viumbe vya mbinguni, na wakaaji wa dunia; hakuna anayeweza kumupinga, au kusema: Unafanya nini?


Ee mufalme, Mungu Mukubwa alimupa baba yako mufalme Nebukadneza ufalme, ukubwa, mamlaka na utukufu.


Alifukuzwa mbali na wanadamu, akili yake ikafanywa kama ya nyama, akaishi na punda wa pori, akakuwa anakula majani kama ngombe, na kulowanishwa na umande wa mbinguni mpaka alipotambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye anamupa ufalme ule mutu yeyote anayemutaka.


Halafu mufalme Dario akawaandikia watu wa makabila yote, mataifa yote, na luga zote katika dunia: Ninawatakia amani kwa wingi.


Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme, kusudi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote wamutumikie. Utawala wake ni wa milele na ufalme wake hautaangamizwa hata kidogo.


Ufalme, utawala na ukubwa wa falme zote katika dunia watapewa kwa watu wa watakatifu wa Mungu Mukubwa. Ufalme wao utakuwa wa kudumu milele, na tawala zote zitawatumikia na kuwatii.


Kwa hiyo, ee Yawe, Mungu wetu, ulikuwa tayari kutuazibu, na ukafanya hivyo, kwa sababu unafanya mambo yanayokuwa ya haki, nasi hatukukusikiliza.


Basi, wakamulilia Yawe wakisema: Ee Yawe, tunakusihi usituangamize kwa kuutoa uzima wa mutu huyu, wala usituazibu kwa kumwanga damu ya mutu asiyekuwa na kosa. Wewe, ee Yawe, umefanya unavyopenda.


Hao waliolemewa ndio watakaobaki wazima; hao waliopelekwa katika uhamisho watakuwa taifa lenye nguvu. Yawe atawatawala kwenye mulima Sayuni, tangu wakati ule na hata milele.


Yeye atatawala taifa la Israeli hata milele, nao ufalme wake hautakuwa na mwisho.”


Lakini yule mulipishaji wa kodi alisimama kwa mbali, naye hakusubutu hata kuinua macho yake kuelekea mbingu; lakini alijipigapiga kwa huzuni na kusema: ‘Ee Mungu, unisamehe mimi mutenda mabaya.’ ”


Kama vile Baba ana uwezo wa kupana uzima, ndivyo vilevile amemupa Mwana uwezo wa kupana uzima.


Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.


Kwa Mufalme wa milele, asiyeweza kufa, asiyeonekana, Mungu peke yake, ikuwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.


Ni yeye tu asiyeweza kufa na anayekaa katika mwangaza ambao mutu hawezi kukaribia. Hakuna mutu aliyemwona wala hakuna mutu anayeweza kumwona. Ndiye mwenye heshima na uwezo wa milele! Amina.


Akaapa kwa jina la Mungu anayeishi kwa milele na milele, muumba wa mbingu na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake, nayo dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, pamoja na bahari na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake, na kusema: “Hakutakuwa tena muda unaobaki!”


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


wale wazee makumi mbili na wane waliinama uso mpaka chini mbele ya yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakimwabudu huyo anayeishi kwa milele na milele. Nao walikuwa wakikuja kuweka taji zao mbele ya kiti chake, na kusema:


Vile viumbe vine vya ajabu viliimba kwa kumutukuza, kumuheshimia na kumushukuru yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme, yule anayeishi kwa milele na milele. Kila mara vilipofanya vile,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ