Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 4:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Wakaaji wote wa dunia si kitu; anafanya anavyotaka na viumbe vya mbinguni, na wakaaji wa dunia; hakuna anayeweza kumupinga, au kusema: Unafanya nini?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 4:32
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alimusihi, naye Mungu akapokea maombi yake na kusihi kwake, akamurudisha Yerusalema katika ufalme wake. Halafu Manase akatambua kwamba Yawe ndiye Mungu.


Ninajua kwamba unaweza kila kitu, lolote unalokusudia haliwezi kuzuiliwa.


Yeye akitwaa kitu kwa rafla, nani anayeweza kumuzuia? Nani anayeweza kumwuliza: “Unafanya nini?”


Mungu wetu yuko mbinguni; yeye anafanya yote anayotaka.


Yawe anafanya chochote anachotaka, mbinguni, katika dunia, ndani ya bahari na shimo ndefu.


Watu wakawakusanya vyura wale malundomalundo. Inchi nzima ikanuka.


Maana mara hii, wewe mwenyewe, wakubwa wako na watu wako mutapatwa na mapigo yangu makali. Nawe utatambua kwamba hakuna yeyote katika dunia anayekuwa kama mimi.


Musa akamwambia: “Mara tu nitakapotoka inje ya muji nitainua mikono na kumwomba Yawe. Ngurumo itakoma na hakutakuwa mvua ya mawe tena kusudi utambue kwamba dunia ni ya Yawe.


Sasa, ee Yawe, Mungu wetu, utuokoe toka katika makucha ya Saniharibu, kusudi falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe peke yako, ee Yawe, ambaye ni Mungu.”


Kwake mataifa ni kama tone la maji katika mbeketi, ni kama mavumbi juu ya kilo. Kwake visanga ni vyepesi kama mavumbi laini.


Mataifa yote si kitu mbele yake; kwake ni vitu vya ovyo na bure kabisa.


Nitakupa akiba zilizofichwa na mali inayokuwa pahali pa siri, upate kutambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wa Israeli, ninayekuita kwa jina lako.


Ni mimi niliyeumba dunia, watu na nyama wanaokuwa ndani yake kwa uwezo wangu na kwa nguvu zangu kubwa. Nami ninaitoa kwa yeyote ninayetaka.


Anabadilisha nyakati na wakati, anaondoa na kuwatawalisha wafalme. Anawapa hekima wenye hekima, anawaongezea wenye maarifa ufahamu.


Kwa mwisho wa ile miaka saba, mimi Nebukadneza niliinua macho yangu kuangalia juu mbinguni na akili zangu zikanirudilia. Nilimushukuru Mungu Mukubwa na kumuheshimu yeye anayeishi milele: Kwa sababu mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ufalme wake unadumu kwa vizazi vyote.


Alifukuzwa mbali na wanadamu, akili yake ikafanywa kama ya nyama, akaishi na punda wa pori, akakuwa anakula majani kama ngombe, na kulowanishwa na umande wa mbinguni mpaka alipotambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye anamupa ufalme ule mutu yeyote anayemutaka.


kusudi watu wote wa dunia wajue kwamba mukono wa Yawe una nguvu; nanyi mupate kumwogopa Yawe, Mungu wenu, milele.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ