Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 4:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 basi, ni wewe, ee mufalme, ambaye umekuwa mukubwa na mwenye nguvu. Ukubwa wako umefika mpaka mbinguni, na ufalme wako umeenea mpaka miisho ya dunia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 4:19
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Rakeli akamwambia baba yake: “Tafazali baba, usiuzike, maana siwezi kusimama mbele yako kwa sababu niko katika siku zangu.” Basi, Labani akatafuta sanamu za miungu yake, lakini hakuzipata.


Akamwagiza yule aliyetangulia: “Ndugu yangu Esau atakapokutana nawe na kukuuliza: ‘Wewe ni mutumishi wa nani? Unakwenda wapi? Na nyama hawa ni wa nani?’


Yosefu akamwambia yule mutumishi: “Tafsiri ya ndoto yako ni hii: yale matawi matatu ni siku tatu.


Obadia alipokuwa katika njia, alikutana na Elia; naye Obadia alipomutambua Elia, aliinama chini na kusema: “Hakika, ni wewe bwana wangu Elia?”


Lakini sasa, ninakuomba uwasamehe zambi yao. Ikiwa hautawasamehe, ninakusihi unifute mimi katika kitabu chako ambamo uliwaandika watu wako.


Mushugulike na kuleta ustawi katika muji ule ambamo nimewahamishia. Muuombee muji huo kwa Yawe, maana ukistawi ninyi vilevile mutastawi.


Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.


Yule mukubwa wa watumishi akawapa majina mengine; akamwita Danieli kwa jina la Beltesaza, Hanania kwa jina la Sadiraki, Misaeli kwa jina la Mesaki na Azaria kwa jina la Abedenego.


Mufalme akamwuliza Danieli, ambaye vilevile aliitwa Beltesaza: Unaweza kunijulisha ndoto niliyoota na maana yake?


Wewe, ee mufalme, mufalme wa wafalme! Mungu amekupa ufalme, uwezo, nguvu na utukufu!


Kwa sababu hiyo, ee mufalme, sikiliza shauri langu. Achana na zambi zako na maovu yako, utende haki na kuwaonea huruma walioteswa; labda muda wako wa kufanikiwa utarefushwa!


kwa sababu ana roho njema, maarifa, ujuzi wa kufasiria ndoto, kufumbua mafumbo na kutatua matatizo. Jina la mutu huyo ni Danieli ambaye baba yako alimwita Beltesaza. Basi wamwite, naye atakuelezea maana ya maandiko haya.


Ee mufalme, Mungu Mukubwa alimupa baba yako mufalme Nebukadneza ufalme, ukubwa, mamlaka na utukufu.


Kwa sababu ya ukubwa aliomupa, watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote walitetemeka na kumwogopa. Nebukadneza aliweza kumwua mutu yeyote aliyetaka na kumwacha muzima mutu yeyote aliyetaka. Aliyetaka kumupandisha cheo alimupandisha, aliyetaka kumushusha cheo alimushusha.


Maono niliyoyaona mimi Danieli yaliniogopesha, nami nikafazaika.


Huu ndio mwisho wa jambo hilo. Mawazo yangu yaliniogopesha sana mimi Danieli, hata rangi yangu ikabadilika. Lakini nilichunga jambo hilo ndani ya moyo wangu.


Mimi Danieli, nikazimia na kuugua kwa muda. Nilipopona, nikaendelea na shuguli za mufalme. Lakini yale maono yalishangaza, nami sikuweza kuyaelewa.


Milima ilikuona, ikanyauka; mafuriko ya maji yakapita mule. Vilindi vya bahari vilinguruma, na kurusha juu mawimbi yake.


Lakini Hana akamujibu: “Sivyo bwana wangu. Mimi ni mwanamuke mwenye taabu sana; mimi sijakunywa divai wala kinywaji kikali, lakini nimekuwa nikimutolea Yawe yanayokuwa ndani ya roho yangu.


Kwa maneno hayo, Daudi akawashawishi watu wake wasimuzuru Saulo; aliwakataza wasimushambulie. Kisha Saulo akasimama, akatoka ndani ya pango akaendelea na safari yake.


Daudi akamujibu: “Wewe si mwanaume? Nani anayekuwa sawa nawe katika Israeli? Mbona basi, haukumulinda bwana wako mufalme? Mutu mumoja kati yetu aliingia pale kwa kumwangamiza bwana wako mufalme!


Eli akamwuliza: “Yawe alikuambia nini? Usinifiche alichokuambia. Ikiwa utanificha kitu alichokuambia, Mungu akuazibu vikali.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ