Tena alipogundua kwamba Mordekayi alikuwa Muyuda, akaamua kwamba kumwazibu peke yake haitoshi. Basi akafanya shauri la kuwaangamiza Wayuda wote, watu wa ukoo wa Mordekayi, katika utawala wa mufalme Ahasuero.
Mufalme alitaka vijana wasiokuwa na kilema, wazuri kwa umbo, wenye ujuzi wa kila hekima, wenye akili na maarifa na wanaofaa kwa kutumika katika nyumba ya kifalme. Alitaka vilevile vijana wale wafundishwe kusoma na kuandika luga ya Wakaldea.
Wale Wakaldea wakamujibu: Mufalme, hakuna mutu yeyote katika dunia anayeweza kutimiza mapenzi yako. Hakuna mufalme yeyote, hata akuwe mukubwa na mwenye nguvu yapata gani aliyepata kuwauliza waganga au walozi au Wakaldea jambo kama hilo.
Kwa hiyo, watu wote, mara tu waliposikia sauti za baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, walianguka uso mpaka chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu ambayo mufalme Nebukadneza alisimamisha.
Danieli akaonekana kuwa bora kuliko wale wasimamizi wengine na wakubwa wote kwa maana alikuwa na roho njema. Hivyo mufalme akakusudia kumupa uongozi wa ufalme wote.