Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 3:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Basi, mufalme Nebukadneza akawapandishia vyeo Sadiraki, Mesaki na Abedenego katika jimbo la Babeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 3:30
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya vijito, unaozaa matunda kwa wakati wake, na majani yake hayanyauki hata kidogo. Anafanikiwa katika yote anayofanya.


Mungu anasema: “Nitamwokoa yule anayenipenda; nitamulinda anayejua jina langu!


Yule mukubwa wa watumishi akawapa majina mengine; akamwita Danieli kwa jina la Beltesaza, Hanania kwa jina la Sadiraki, Misaeli kwa jina la Mesaki na Azaria kwa jina la Abedenego.


Danieli akamwomba mufalme, naye mufalme akawaweka Sadiraki, Mesaki na Abedenego kuwa wasimamizi wa mambo ya utawala ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli akabakia katika nyumba ya mufalme.


Mufalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya zahabu, yenye urefu wa metre makumi mbili na nane na upana wa metre tatu. Akaisimamisha katika bonde la Dura katika jimbo la Babeli.


Sasa, kuna Wayuda fulani uliowachagua kwa kushugulikia mambo ya utawala wa jimbo la Babeli, nao ni: Sadiraki, Mesaki na Abedenego; watu hawa, ee mufalme, hawakutii amri yako. Wanakataa kuitumikia miungu yako na kuiabudu ile sanamu ya zahabu uliyoisimamisha.


Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ