Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 3:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Basi, mufalme Nebukadneza akaukaribia mulango wa furu la moto mukali, akaita: Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watumishi wa Mungu Mukubwa, mutoke mukuje hapa! Sadiraki, Mesaki na Abedenego wakatoka ndani ya moto.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 3:26
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye Melkisedeki, mufalme wa muji wa Salemu, ambaye alikuwa kuhani wa Mungu Mukubwa, akaleta mukate na divai,


maana ni watu wako, na ni mali yako, watu ambao uliwatoa Misri kutoka katika furu ya chuma.


Wao wakatujibu hivi: “Sisi ni watumishi wa Mungu wa mbingu na dunia, na tunaijenga upya nyumba ambayo ilikuwa imejengwa na kumalizika pale mbele na mufalme mumoja mukubwa wa Israeli.”


Umewaacha watu watukanyage; tumepitia katika moto na katika maji. Lakini sasa umetuleta kwenye usalama.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.


Mara hii hamutatoka kwa haraka, wala hamutaondoka mbiombio! Maana Yawe atawatangulia, Mungu wa Israeli atawalinda nyuma yenu.


Hili ni agano nililowaagiza babu zenu kutii nilipowaondoa katika inchi ya Misri, kutoka katika shimo la moto. Niliwaambia wanitii na kufanya yote niliyowaamuru, na kwamba wakifanya hivyo, watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.


Mufalme akamwambia Danieli: Hakika, Mungu wako ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme, na ndiye anayefumbua mafumbo kwa sababu ameweza kunifumbulia fumbo hili.


Mungu wetu ambaye tunamutumikia anaweza kutuokoa. Atatuokoa kutoka furu la moto mukali na vilevile kutoka katika mikono yako, ee mufalme.


Lakini nikaota ndoto iliyonitisha; nikiwa nimelala katika kitanda, mawazo na maono yaliniogopesha.


Ilipokuwa asubui mapema, mufalme Dario aliamuka, akaenda kwa haraka kwenye pango la simba.


Alipofika karibu akamwita Danieli kwa sauti ya huzuni: Danieli, mutumishi wa Mungu Mwenye Uzima, Mungu wako unayemutumikia siku zote ameweza kukuokoa na simba hawa?


Huyo atasema maneno ya kujivuna mbele ya Mungu Mukubwa na kuwatesa watakatifu wake. Atajaribu kubadilisha sikukuu na sheria zao, na watakatifu watatiwa katika mikono yake kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


Mwanamuke yule akaendelea kumufuata Paulo na sisi, akilalamika akisema: “Watu hawa ni watumishi wa Mungu Mukubwa. Wanawatangazia ninyi namna gani munavyoweza kuokolewa.”


Lakini Paulo akawaambia wajumbe: “Wametupiga mbele ya watu wote bila kutusambisha, ijapokuwa sisi ni wanainchi wa Roma, na kisha wakatutia ndani ya kifungo. Na sasa namna gani wanataka kututosha kwa uficho? Haiwezekani! Wao wenyewe wafike kutufungua!”


Kwa maana usiku malaika wa Mungu, ninayekuwa mutu wake na ninayemwabudu, alinitokea


Basi kusema vile inaonyesha kwamba ninatafuta watu wanikubali? Hapana! Ninataka kukubaliwa na Mungu. Au ninatafuta kuwapendeza watu? Kama ningekuwa ningali ninatafuta kuwapendeza watu, singekuwa mutumishi wa Kristo.


Lakini ninyi ndio watu aliowakomboa kutoka Misri katika furu la chuma. Aliwatoa huko kusudi mukuwe watu wake kama vile munavyokuwa hivi leo.


Wakati Waisraeli walipokuwa wanavuka, makuhani waliokuwa wanalibeba Sanduku la Agano walisimama pahali pakavu katikati ya muto Yordani mpaka taifa lote likavuka.


Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano, walisimama katikati ya muto Yordani mpaka watu walipomaliza kutimiza kila kitu ambacho Yawe alimwamuru Yoshua awaambie watu; Yoshua alifanya yote ambayo Musa alikuwa amemwamuru. Watu wakaharakisha kuvuka muto,


Kisha sauti ikasikilika toka kwenye kiti cha kifalme ikasema: “Mumusifu Mungu wetu ninyi watumishi wake wote, ninyi wote munaomuheshimu, wakubwa na wadogo!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ