Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 3:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Na kwamba mutu yeyote asiyeinama chini na kuiabudu sanamu hiyo, atupwe ndani ya furu la moto mukali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 3:11
6 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe, ee mufalme, ulitoa amri kwamba kila mutu anaposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na kila aina ya muziki, ainame chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu.


Sasa, kuna Wayuda fulani uliowachagua kwa kushugulikia mambo ya utawala wa jimbo la Babeli, nao ni: Sadiraki, Mesaki na Abedenego; watu hawa, ee mufalme, hawakutii amri yako. Wanakataa kuitumikia miungu yako na kuiabudu ile sanamu ya zahabu uliyoisimamisha.


Na yeyote ambaye hatainama chini na kuiabudu, atatupwa mara moja katika furu la moto mukali.


Basi, walikwenda kwa mufalme na kumushitaki Danieli kwa kutumia ile sheria, wakisema: Mufalme Dario, haukutia sahihi kwenye sheria kwamba kwa muda wa siku makumi tatu hakuna mutu yeyote atakayeruhusiwa kuomba kitu chochote, kwa mungu yeyote, au kwa mutu yeyote isipokuwa kutoka kwako wewe, ee mufalme, na kwamba yeyote atakayevunja sheria hii atatumbukizwa katika pango la simba? Mufalme akaitikia: Hivi ndivyo inavyokuwa kulingana na sheria ya Wamedi na Wapersi ambayo haiwezi kuvunjika.


Basi, hao wakubwa na maliwali wote pamoja, wakamwendea mufalme na kumwambia: Uishi milele ee mufalme Dario!


“Tulikuta kifungo kimefungwa vizuri na waaskari walinzi wakichunga milango. Lakini wakati tulipofungua milango hatukuona mutu ndani.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ